Waziri wa Biashara na Viwanda wa Jamhuri ya Niger amesisitiza kuhusu kuimarishwa uhusiano baina ya nchi yake na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika nyanja mbalimbali zikiwemo za kiuchumi.
Maidani ya usafiri wa umma katika mji wa Agadez huko kaskazini mwa Niger imekuwa ikishuhudia wimbi la watu wanaowasili na kuondoka tangu utawala wa kijeshi wa nchi hiyo ubatilishe amri ya kupiga marufuku usafirishaji wa wahamiaji haramu na shughuli zote zinazohusiana na wahajiri huko Niger Novemba mwaka jana.
Baada ya kugonga mwamba mazungumzo ya kisiasa ya Marekani ya kudumisha uwepo wake wa kijeshi nchini Niger, kwa mara nyingine tena raia katika nchi hiyo ya Kiafrika wametoa mwito wa kuondoka kwa wanajeshi wa Marekani katika nchi yao kwa kufanya maandamano mbele ya kambi ya kijeshi ya Marekani kaskazini mwa Niger.
Mamia ya watu wameshiriki katika maandamano ya kupinga uwepo wa majeshi ya kigeni nchini Niger, vikiwemo vikosi vya jeshi vya Marekani ambayo ina kambi ya kijeshi kaskazini mwa nchi hiyo.
Amadou Abdurrahman, Msemaji wa Serikali ya Niger, ametangaza kupitia taarifa kwamba nchi hiyo imefuta makubaliano yote ya kijeshi na Marekani ambayo yaliruhusu nchi hiyo ya Magharibi kuweka majeshi yake katika ardhi ya Niger.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesisitiza kuwa serikali ya Rais Ebrahim Raisi ina hamu ya kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano na nchi za Afrika ikiwemo Niger.
Serikali ya Niger imetangaza kwamba "bila kupoteza muda" inavunja makubaliano yake ya ushirikiano wa kijeshi na Marekani.
Mali, Niger na Burkina Faso zimetangaza habari ya kuunda kikosi cha pamoja cha jeshi kitakachosaidia kukabiliana na utovu wa usalama uliosababishwa na harakati za makundi ya kigaidi katika nchi hizo za Afrika Magharibi.
Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS) imeamua kuondoa vikwazo ilivyokuwa imeiwekea Guinea.
Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Magharibi mwa Afrika ECOWAS imetangaza habari ya kuiondolea Niger vikwazo vya kiuchumi na kifedha.