-
Jeshi la Sudan Kusini: Tumeukomboa mji muhimu kutoka mikononi mwa Jeshi Jeupe
Apr 22, 2025 08:46Jeshi la Sudan Kusini limetangaza kuwa limeukomboa mji muhimu katika jimbo la Upper Nile ambao ulikuwa umetekwa na wanamgambo wa kabila la Nuer mwezi Machi katika mapigano ambayo yalipelekea kuwekwa kwenye kizuizi cha nyumbani Makamu wa Kwanza wa Rais Riek Machar na kuibua mzozo mkubwa wa kisiasa nchini humo.
-
Makumi wauawa katika shambulio la wabeba silaha Nigeria
Apr 14, 2025 13:08Zaidi ya watu 40 wameuawa katika shambulio la usiku wa manane dhidi ya jamii ya Zike huko Bassa, Jimbo la Plateau, huku mashambulio makali ya makundi yenye silaha yakiendelea kuripotiwa katika eneo hilo la kaskazini ya kati mwa Nigeria.
-
Watu 8 wameuawa na 11 kujeruhiwa katika mlipuko wa Boko Haram kaskazini mashariki mwa Nigeria
Apr 13, 2025 12:18Takriban watu wanane wameuawa na wengine 11 kujeruhiwa wakati basi moja katika Jimbo la Borno nchini Nigeria lilipokanyaga bomu lililotegwa ardhini na magaidi wa Boko Haram.
-
Wanahabari Nigeria wataka Israel iwekewe vikwazo vya mafuta, gesi
Apr 10, 2025 02:53Mwenyekiti wa Muungano wa Waandishi wa Habari wa Nigeria (NUJ), Ibrahim Muhammad, ametoa wito kwa nchi za Kiislamu kuungana na kutumia nguvu zao za kiuchumi, hususan mafuta na gesi, kama nyenzo ya kukomesha mauaji ya kimbari ya Israel na Marekani huko Palestina na kwingineko.
-
Lassa yaua watu 118 Nigeria ndani ya miezi mitatu
Apr 01, 2025 10:35Homa ya Lassa imeua watu 118 nchini Nigeria katika kipindi cha miezi mitatu ya kwanza ya mwaka huu. Hayo yamesemwa na Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa cha nchi hiyo ya Afrika Magharibi (NCDC).
-
Ukatili wa Polisi Dhidi ya Waandamanaji wa Siku ya Kimataifa Quds Nchini Nigeria
Apr 01, 2025 02:39Katika maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds yaliyofanyika nchini Nigeria Ijumaa kwa kushirikisha mamia ya Waislamu na wanachama wa Harakati ya Kiislamu ya nchi hiyo – kwa lengo la kuonyesha mshikamano na watu wa Palestina na kulaani uhalifu wa utawala wa Kizayuni wa Israel– maafisa wa polisi wa Nigeria walifyatua risasi dhidi ya waandamanaji. Tukio hilo lilisababisha waandamanaji wasiopungua 18 kuuawa shahidi, wengine kujeruhiwa, na wengi kukamatwa.
-
Nigeria yalaaniwa kwa kukandamiza waandamanaji wa Siku ya Quds
Mar 30, 2025 11:12Baraza la Uratibu wa Tablighi ya Kiislamu la Iran limetoa taarifa ya kulaani ukandamizaji waliofanyiwa Waislamu wa Nigeria wakati wa kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Quds na kuandika: "Ukandamizaji na kumwagwa damu za waandamanaji wa Siku ya Kimataifa ya Quds nchini Nigeria na kuuawa shahidi kidhulma Waislamu 18 waliokuwa kwenye saumu ya Ramadhani kunaonesha hofu ya watawala wa Nigeria kuhusu mwamko wa Waislamuj na nafasi ya kiistratijia ya Siku ya Kimataifa ya Quds duniani."
-
Magaidi washambulia kambi za jeshi Nigeria, Cameroon na kuua askari 16
Mar 27, 2025 11:08Watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa magenge ya kigaidi wamefanya mashambulizi yaliyoratibiwa dhidi ya kambi ya jeshi la Cameroon karibu na Ziwa Chad na dhidi ya kituo cha kijeshi kaskazini mashariki mwa Nigeria, na kuua takriban wanajeshi 16.
-
Nigeria yathibitisha vifo vipya vitano kutokana na homa ya Lassa
Mar 13, 2025 02:21Nigeria imethibitisha vifo vipya vitano kutokana na homa ya Lassa, ugonjwa ambao umesambaa katika eneo la magharibi mwa Afrika.
-
Mripuko wa homa ya uti wa mgongo waua makumi Nigeria
Mar 12, 2025 07:05Watu wasiopungua 26 wameaga dunia kutokana na mripuko wa ugonjwa wa uti wa mgongo (Meningitis) katika Jimbo la Kebbi kaskazini magharibi mwa Nigeria.