-
Raia zaidi ya 300 waliotekwa nyara Nigeria waokolewa katika operesheni kubwa
Aug 06, 2026 11:02Nigeria imesema kuwa zaidi ya watu 300 waliotekwa nyara katika mashambulizi tofauti ya watu wenye silaha wameokolewa kupitia operesheni ya pamoja ya kiintelijensia na kiusalama.
-
Watu wenye silaha waua raia wasiopungua 30 jimboni Kaduna, Nigeria
Jul 28, 2026 14:02Watu wasiopungua 30 wameuawa wakati genge la wenye silaha liliposhambulia kijiji kimoja katika jimbo la Kaduna kaskazini magharibi mwa Nigeria. Hayo yamethibitishwa na wakazi wawili wa kijiji hicho.
-
Wakulima 26 wazikwa baada ya shambulio la majambazi kaskazini-magharibi mwa Nigeria
Jul 25, 2026 11:05Wakulima 26 waliouawa katika shambulio la majambazi katika Jimbo la Zamfara, kaskazini-magharibi mwa Nigeria, walizikwa siku ya Ijumaa.
-
UNICEF yahimiza ulinzi wa watoto wakati wa migogoro ya usalama na binadamu
Jul 18, 2026 11:51Mkuu wa Shirika la Watoto la Umoja wa Mataifa (UNICEF) ametembelea kaskazini magharibi mwa Nigeria, wakati migogoro, umaskini na ukosefu wa usalama wa chakula vikiwalazimisha mamilioni ya watoto katika eneo hilo kuhitaji msaada ya dharura.
-
Mkuu wa wakala bandia wa serikali ya Nigeria akamatwa baada ya kuwa mafichoni kwa wiki kadhaa
Jul 15, 2026 15:36Polisi ya Nigeria imemtia mbaroni mtu aliyeanzisha wakala bandia wa serikali uliokuwa ukifanyia kazi zake katika ofisi ya Rais kwa karibu miaka miwili.
-
UN: Kutoadhibiwa wahalifu kunaeneza hisia za mauaji ya kimbari nchini Nigeria
Jun 21, 2026 02:52Ripoti ya Umoja wa Mtaifa inasema, kutoadhibiwa watu wanaofanya mashambulizi ya mara kwa mara dhidi ya viongozi wa kidini na sehemu za ibada, pamoja na kinga dhaifu na uwajibikaji duni, vinawafanya waathiriwa nchini Nigeria kuona kwamba vurugu zinazofanyika nchini humo ni mateso au hata mauaji ya halaiki.
-
Nigeria: Karibu wapiganaji 10,000 wa zamani wa Boko Haram waunganishwa katika jamii
Jun 16, 2026 11:00Mamlaka husika katika Jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa Nigeria zimearifu kuwa karibu wapiganaji 10,000 wa zamani wa kundi la waamgambo wa Boko Haram sasa wameunganishwa tena katika jamii chini ya mpango unaofadhiliwa na serikali wa kurekebisha tabia na kuhimiza kuachana na makundi ya uasi.
-
Rais wa Nigeria atangaza mauaji ya wapiganaji 13,000 mwaka jana
Jun 12, 2026 12:36Rais wa Nigeria, Bola Ahmed Tinubu, ametangaza leo Ijumaa kwamba "magaidi" wasiopungua 13,000 waliuawa nchini Nigeria mwaka jana, akisisitiza kwamba idadi ya vifo vinavyotokana na uasi wa kutumia silaha nchini humo imepungua kwa 81% tangu alipochukua madaraka Mei 2023.
-
Nigeria: Mamia ya wanawake na watoto waliotekwa nyara na magaidi waachiliwa
Jun 08, 2026 03:12Mamia ya wanawake na watoto waliokuwa wametekwa nyara na kundi la kigaidi la Boko Haram kaskazini mashariki mwa Nigeria wameachiwa huru mwishoni mwa wiki.
-
Jeshi la Nigeria laangamiza magaidi 50, yumo kamanda mkuu wa kundi la ISWAP
Jun 04, 2026 03:05Wanajeshi wa Nigeria wanaoendesha oparesheni kwa jina "Hadin Kai" wamewaangamiza magaidi wasiopungua 50, akiwemo kamanda mkuu wa tawi la ISWAP lililoungana na kundi la Boko Haram.