-
Waislamu Nigeria wawakumbuka Mashahidi wa Siku ya Quds
May 12, 2025 11:14Taasisi ya 'Wakfu wa Shuhada' ya Harakati ya Kiislamu ya Nigeria imewakumbuka na kuwaenzi mashahidi 27 waliouawa na vikosi vya jeshi la nchi hiyo wakati wa maandamano ya amani ya Siku ya Quds ya 2025 huko Abuja, na kusisitiza kujitolea kwao kwa kadhia ya Palestina.
-
Makumi wauawa katika mashambulizi ya wabeba silaha Benue, Nigeria
May 12, 2025 11:10Takriban watu 23 waliuawa huku wengine wengi kujeruhiwa katika mashambulizi ya watu waliojizatiti kwa silaha katika Jimbo la Benue nchini Nigeria.
-
Makamanda 11 wa ugaidi wauawa katika operesheni za jeshi la Nigeria
May 08, 2025 07:04Takriban vinara 11 wa magenge ya kigaidi nchini Nigeria wameuawa na vikosi vya serikali katika operesheni za kupambana na ugaidi katika nchi hiyo yenye watu wengi zaidi barani Afrika.
-
Nigeria yageukia Akili Mnemba (AI) ili kukabiliana na taarifa za uongo na kukuza lugha za ndani
May 08, 2025 02:22Huku Akili Mnemba (AI) ikiendelea kuhuhisha sekta ya viwanda kote duniani, Nigeria nchi iliyo na uchumi mkubwa zaidi barani Afrika imeamua kukumbatia kwa kasi wimbi hili la kiteknolojia.
-
Jeshi la Sudan Kusini: Tumeukomboa mji muhimu kutoka mikononi mwa Jeshi Jeupe
Apr 22, 2025 08:46Jeshi la Sudan Kusini limetangaza kuwa limeukomboa mji muhimu katika jimbo la Upper Nile ambao ulikuwa umetekwa na wanamgambo wa kabila la Nuer mwezi Machi katika mapigano ambayo yalipelekea kuwekwa kwenye kizuizi cha nyumbani Makamu wa Kwanza wa Rais Riek Machar na kuibua mzozo mkubwa wa kisiasa nchini humo.
-
Makumi wauawa katika shambulio la wabeba silaha Nigeria
Apr 14, 2025 13:08Zaidi ya watu 40 wameuawa katika shambulio la usiku wa manane dhidi ya jamii ya Zike huko Bassa, Jimbo la Plateau, huku mashambulio makali ya makundi yenye silaha yakiendelea kuripotiwa katika eneo hilo la kaskazini ya kati mwa Nigeria.
-
Watu 8 wameuawa na 11 kujeruhiwa katika mlipuko wa Boko Haram kaskazini mashariki mwa Nigeria
Apr 13, 2025 12:18Takriban watu wanane wameuawa na wengine 11 kujeruhiwa wakati basi moja katika Jimbo la Borno nchini Nigeria lilipokanyaga bomu lililotegwa ardhini na magaidi wa Boko Haram.
-
Wanahabari Nigeria wataka Israel iwekewe vikwazo vya mafuta, gesi
Apr 10, 2025 02:53Mwenyekiti wa Muungano wa Waandishi wa Habari wa Nigeria (NUJ), Ibrahim Muhammad, ametoa wito kwa nchi za Kiislamu kuungana na kutumia nguvu zao za kiuchumi, hususan mafuta na gesi, kama nyenzo ya kukomesha mauaji ya kimbari ya Israel na Marekani huko Palestina na kwingineko.
-
Lassa yaua watu 118 Nigeria ndani ya miezi mitatu
Apr 01, 2025 10:35Homa ya Lassa imeua watu 118 nchini Nigeria katika kipindi cha miezi mitatu ya kwanza ya mwaka huu. Hayo yamesemwa na Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa cha nchi hiyo ya Afrika Magharibi (NCDC).
-
Ukatili wa Polisi Dhidi ya Waandamanaji wa Siku ya Kimataifa Quds Nchini Nigeria
Apr 01, 2025 02:39Katika maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds yaliyofanyika nchini Nigeria Ijumaa kwa kushirikisha mamia ya Waislamu na wanachama wa Harakati ya Kiislamu ya nchi hiyo – kwa lengo la kuonyesha mshikamano na watu wa Palestina na kulaani uhalifu wa utawala wa Kizayuni wa Israel– maafisa wa polisi wa Nigeria walifyatua risasi dhidi ya waandamanaji. Tukio hilo lilisababisha waandamanaji wasiopungua 18 kuuawa shahidi, wengine kujeruhiwa, na wengi kukamatwa.