-
Shambulio la anga la Nigeria laua watoto saba, lajeruhi watano nchini Niger
Feb 21, 2022 07:44Watoto saba wameuawa na wengine watano wamejeruhiwa katika shambulio la anga ambalo imeelezwa kuwa limefanywa kimakosa na jeshi la Nigeria katika eneo la Maradi kusini mwa Niger.
-
Turathi zilizoibiwa na mkoloni Muingereza zarejeshwa Nigeria baada ya karne
Feb 20, 2022 07:56Turathi mbili muhimu za kihistoria za Nigeria zilizoibiwa na Uingereza katika enzi za ukoloni hatimaye zimerejeshwa katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi, baada ya kupita zaidi ya miaka mia moja.
-
Waislamu Nigeria waandamana kulaani mauaji ya kimbari ya utawala wa Saudi Arabia nchini Yemen
Feb 19, 2022 07:43Waislamu nchini Nigeria wakiitikia wito wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria wameandamana katika mji mkuu wa nchi hiyo Abuja, kulaani jinai za muungano vamizi unaoongozwa na utawala wa Saudi Arabia ambao umeendelea kutenda jinai na mauaji ya kimbari nchini Yemen.
-
Watu 17 wafariki dunia katika mlipuko wa lori la mafuta nchini Nigeria
Feb 19, 2022 07:39Kwa akali watu 17 wamepoteza maisha yao katika tukio la mlipuko wa lori la mafuta katika jimbo la Ogun, kusini magharibi mwa Nigeria
-
Nigeria yasajili vifo 59 vya homa ya Lassa tokea Januari 3
Feb 18, 2022 03:08Watu wasiopungua 59 wameripotiwa kupoteza maisha kutokana na mripuko mpya wa homa ya Lassa katika sehemu mbalimbali za Nigeria tokea Januari 3 mwaka huu hadi sasa.
-
Sheikh Ibrahim Zakzaky: Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran ni ya Waislamu wote ulimwenguni
Feb 07, 2022 12:51Sheikh Ibrahim Zakzaky, Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria amesema kuwa, Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran hayaishii tu katika mipaka ya Iran na wananchi wa taifa hili bali ni mali ya Waislamu wote ulimwenguni.
-
Sheikh Zakzaky awataka walimwengu wakabiliane na mashambulio ya Saudia dhidi ya Yemern
Feb 06, 2022 04:42Sheikh Ibrahim Zakzaky, Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria amewataka walimwengu kujitokeza na kukabiliana na hujuma na mashambulio ya muungano vamizi unaoongozwa na Saudi Arabia dhidi ya wananchi madhulumu wa Yemen.
-
Polisi ya Nigeria yadai kukomboa mateka 94 kutoka kwa magenge ya wahalifu
Feb 03, 2022 08:04Polisi ya Nigeria imetangaza kuwa watu 94 wameokolewa baada ya kuchukuliwa mateka na makundi yenye silaha katika majimbo ya Zamfara, Niger na Katsina.
-
Watu 220 wameuawa Nigeria tangu mwaka huu uanze
Jan 20, 2022 04:25Kwa akali watu 220 wameuawa katika mashambulio ya magenge ya kigaidi na makundi ya uhalifu na ujambazi katika jimbo la Niger nchini Nigeria.
-
Majambazi waua raia 50 nchini Nigeria
Jan 17, 2022 08:01Majambazi wameshambulia kijiji kimoja kaskazini mashariki mwa Nigeria na kuua raia 50 huku magenge ya wahalifu yakiendelea kutekeleza mauaji katika nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika.