-
Watu 18 wauawa katika shambulizi la kigaidi Maiduguri
Feb 17, 2018 04:44Magaidi watatu waliokuwa wamejifunga mabomu wameua watu wasiopungua 18 katika mji wa Maiduguri ulioko kaskazini mashariki mwa Nigeria ambao ni makao makuu ya jimbo la Borno lililoathiriwa zaidi na mashambulizi ya kundi la kigaidi la Boko Haram.
-
Makumi wauawa kwa kufyatuliwa risasi na wezi wa mifugo Nigeria
Feb 16, 2018 10:28Makumi ya watu wameripotiwa kuuawa kwa kufyatuliwa risasi na genge la wezi wa mifugo katika jimbo la Zamfara, kaskazini magharibi mwa Nigeria.
-
Maandamano Nigeria kulaani kuuawa shahidi mwanachama wa Harakati ya Kiislamu
Feb 13, 2018 13:15Wanachama wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria (INM) wameshiriki katika maandamanao ya amani kulaani kuuawa shahidi mmoja wa wananchama wa ngazi za juu wa harakati hiyo.
-
Kiongozi wa Boko Haram asema amechoka na anatamani kufa
Feb 08, 2018 10:24Katika kile kinachoonekana ni kupoteza matumaini na kuhisi kufikwa na maji shingoni, kiongozi wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram, Abubakar Shekau amesema amechoshwa na misukosuko na anatamani kufa.
-
Nigeria inaendelea kumzuilia Sheikh Zakzaky kwa amri ya Marekani
Feb 04, 2018 13:06Mwanaharakati wa kisiasa nchini Nigeria amekosoa vikali hatua ya serikali ya Abuja ya kukataa kumuachia huru mwanachuoni mashuhuri wa Kiislamu, Sheikh Ibrahim Zakzaky licha ya agizo la mahakama, na kusisitiza kuwa msomi huyo anaendelea kuzuiliwa kwa amri ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Amnesty: Makumi ya raia wameuawa katika mashambulizi ya anga ya jeshi la Nigeria
Jan 30, 2018 13:08Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limelituhumu jeshi la Nigeria kuwa limeua makumi ya raia katika mashambulizi ya anga ya mwezi uliopita jimboni Adamawa.
-
Wanigeria waendeleza maandamano ya kutaka Sheikh Ibrahim Zakzaky aachiliwe huru
Jan 20, 2018 03:37Wananchi wa Nigeria Ijumaa waliendeleza maandamano ya kutaka serikali ya nchi hiyo imuachilie Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu Sheikh Ibrahim Zakzaky.
-
Rais wa Nigeria asema hajui kama atagombea muhula wa pili
Jan 18, 2018 11:00Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria amesema hajui iwapo atagombea muhula wa pili wa uchaguzi wa rais unaotazamiwa kufanyika mwaka ujao 2019 au la.
-
12 wauawa, 48 wajeruhiwa katika shambulio la Boko Haram nchini Nigeria
Jan 18, 2018 03:41Watu 12 wameuawa na makumi ya wengine wamejeruhiwa katika shambulio la kujilipua kwa bomu lililotekelezwa sokoni katika jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa Nigeria.
-
Waasi wa Niger Delta watishia kuzishambulia taasisi za mafuta
Jan 17, 2018 11:28Kundi la waasi kwa jina la "Walipizaji Kisasi wa Niger Delta" limetishia kuzishambulia taasisi za mafuta za nchi hiyo siku chache zijazo.