-
Wanazuoni wa Kiislamu watoa fatwa; Mataifa ya Kiislamu yaunge mkono Muqawama wa Palestina
Apr 05, 2025 03:49Umoja wa Kimataifa wa Wanazuoni wa Kiislamu (IUMS) umetoa fatwa (agizo la kidini) ukizitaka nchi za Kiislamu kutoa msaada wa haraka wa kijeshi, kifedha na silaha kwa mrengo wa Muqawama wa Palestina, ili kukabiliana na mauaji ya kimbari yanayoendelea kufanywa na utawala katili wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
SEPAH: Muqawama utakomesha uwepo mchafu wa utawala wa Kizayuni
Apr 03, 2025 23:44Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la nchini Iran SEPAH limetoa taarifa na kutangaza kuwa: "Kambi ya Muqawama hususan wanamapambano shupavu na mashujaa wa Palestina hatimaye itamaliza na kuyakatisha maisha ya aibu ya wavamizi wa Palestina."
-
Pezeshkian: Mataifa ya Kiislamu yanaweza kukomesha jinai za Israel
Apr 03, 2025 08:08Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian amesema umoja na mshikamano miongoni mwa mataifa ya Kiislamu unaweza kuwa chachu ya kukomeshwa jinai za kuogofya za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wananchi madhulumu wa Palestina katika Ukanda wa Gaza.
-
Israel yaua Wapalestina wengine karibu 80 Gaza, Guterres asikitika
Apr 03, 2025 03:35Makumi ya Wapalestina wengine wameuawa shahidi katika mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel huko Gaza usiku kucha.
-
Hizbullah: Iran ndiye muungaji mkono mkuu wa kadhia ya Palestina
Mar 30, 2025 03:51Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesisitiza nafasi muhimu ya Iran katika kuunga mkono kadhia ya Palestina ya kukombolewa kuondokana na uchokozi na uvamizi wa Israel huku akiulaani vikali utawala wa Israel kwa ukatili wake katika eneo zima ambao unawezeshwa kwa kiasi kikubwa na uungaji mkono wa Marekani.
-
Wanachuo 300 wapokonywa viza US kwa kuiunga mkono Palestina
Mar 30, 2025 02:59Marekani imebatilisha viza za wanafunzi zaidi ya 300 wa kigeni kwa kuratibu na kushiriki katika maandamano ya kuwanga mkono na kuwatetea wananchi madhulumu wa Palestina katika mabewa ya vyuo vikuu kote nchini humo.
-
Jeshi la Israel lamuua Msemaji wa HAMAS katika muendelezo wa mauaji ya kimbari Ghaza
Mar 27, 2025 02:27Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limemuua shahidi Msemaji wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS Abdel-Latif al-Qanoua, katika shambulio la kigaidi usiku wa manane wa kuamkia leo lililolenga eneo la Jabalia kaskazini, katika Ukanda wa Ghaza.
-
Tunisia yalaaniwa kwa kumkamata mwanachuo aliyepeperusha bendera ya Palestina
Mar 26, 2025 07:42Mwanafunzi mmoja wa Tunisia amekamatwa kwa kuingia uwanjani na kupeperusha bendera ya Palestina wakati wa mechi ya kuwania kufuzu kwa Kombe la Dunia la 2026 katika mji mkuu wa nchi hiyo, Tunis.
-
Mtengeneza filamu mashuhuri ya Palestina iliyoshinda Oscar apigwa na kukamatwa na askari wa Israel
Mar 25, 2025 08:17Hamdan Ballal, mtengeneza filamu mwenza wa Kipalestina wa filamu iliyoshinda tuzo ya Oscar iitwayo Hakuna Ardhi Nyingine (No Other Land) amekamatwa na wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu baada ya kupigwa na kujeruhiwa vibaya sana na walowezi wa Kizayuni. Hayo yameripotiwa na Yuval Abraham aliyeshirikiana naye kutengeneza filamu hiyo.
-
Jeshi katili la Israel laendelea kumwaga damu za Wapalestina Gaza
Mar 24, 2025 23:21Wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel wamewaua shahidi Wapalestina wengine 17 katika mashambulizi ya alfajiri ya leo katika Ukanda wa Gaza, siku moja baada ya kuua shahidi Wapalestina zaidi ya 60 akiwemo ripota wa Al Jazeera, Hossam Shabat katika ukanda huo.