-
Putin ataka jeshi la Russia lipewe kizazi kipya cha silaha
Sep 20, 2018 10:44Rais Vladmir Putin wa Russia amesisitiza udharura wa kukabidhiwa jeshi la nchi hiyo kizazi kipya cha silaha kwa ajili ya kulifanya jeshi hilo kuwa bora zaidi.
-
Russia: Uchokozi wa Israel wa kutuulia watu wetu Syria lazima utajibiwa
Sep 19, 2018 23:16Mbali na Rais Vladimir Putin na viongozi wengine mbalimbali wa kiserikali wa Russia kusisitizia wajibu wa kujibiwa mauaji yaliyofanywa na Israel dhidi ya wanajeshi wa nchi hiyo huko Syria, mkuu wa akademia ya masuala ya jeopolitiki ya Russia naye ametilia mkazo msimamo huo.
-
Putin: Operesheni za anga za Israel zinakiuka uhuru wa kujitawala Syria
Sep 19, 2018 03:22Rais Vladimir Putin wa Russia amesema operesheni za anga za jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel katika anga ya Syria ni ukiukaji wa mamlaka na kujitawala serikali halali ya sasa ya Damascus. Putin amesema hayo huku mgogoro kuhusu ajali ya kutunguliwa ndege ya Russia katika anga ya Syria wakati wa shambulio la utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya nchi hiyo Kiarabu ukiendelea kutokota.
-
Russia yaionya Israel kufuatia kutunguliwa ndege yake katika anga ya Syria
Sep 18, 2018 09:39Kufuatia ajali ya kutunguliwa ndege ya Russia katika anga ya Syria wakati wa shambulio la utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya nchi hiyo, Wizara ya Ulinzi ya Russia imetangaza kuwa inayo haki ya kujibu mapigo kwa Israel kutokana na tukio hilo.
-
Russia: IAEA haina ushahidi wowote wa kuitia hatiani Syria
Sep 17, 2018 23:27Mwakilishi wa kudumu wa Russia katika Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA amesema kuwa, kutoa madai ya uongo kuhusu Syria kunauondolea itibari wakala huo wa atomiki.
-
Russia: Nchi nyingi zinafikiria kubadilishwa sarafu ya Dola ya Marekani katika biashara
Sep 17, 2018 03:17Msemaji wa Rais Vladmir Putin wa Russia amesema kuwa, nchi nyingi za Ulaya na Asia zinafikiria kubadilishwa sarafau ya Dola ya Marekani katika miamala ya kibiashara.
-
Russia yaitaka IAEA kutoa dhamana ya utekelezaji wa JCPOA
Sep 13, 2018 02:52Russia imeutaka Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) itoe dhamani ya utekelezaji wa makubaliano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Russia yataka kuitishwa kikao cha Baraza la Usalama kujadili mkutano wa pande tatu wa Tehran
Sep 11, 2018 05:12Ofisi ya mwakilishi wa Russia katika Umoja wa Mataifa imetoa wito wa kufanyika kikao cha Baraza la Usalama la umoja huo kuchunguza matokeo ya mkutano wa pande tatu wa Tehran kuhusiana na Syria.
-
Russia: Magaidi, White Helmets wakutana kupanga igizo la shambulizi la kemikali Idlib
Sep 09, 2018 03:03Russia imesema magenge ya kigaidi na kundi eti la 'kutoa misaada' la White Helmets linaloungwa mkono na Wamagharibi yamekutana kaskazini magharibi mwa mkoa wa Idlib, kwa shabaha ya kuratibu igizo la hujuma ya kemikali nchini Syria ili kuielekezea kidole cha lawama serikali halali ya Rais Bashar al-Assad.
-
Kuongezeka mivutano baina ya Russia na Magharibi kuhusu tukio la Salisbury
Sep 07, 2018 20:54Kuzushwa upya madai ya kupewa sumu ya kemikali, jasusi Wa zamani wa Russia, Sergei Skripal, na binti yake katika mji wa Salisbury, wa kusini mwa Uingereza mwezi Machi 2018, kumezua mzozo na mivutano mikubwa baina ya nchi za Magharibi na Russia.