Sep 23, 2018 02:42
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani shambulio la kigaidi lililofanywa leo dhidi ya gwaride la vikosi vya ulinzi mjini Ahvaz kusini magharibi mwa nchi na kueleza kwamba: Iran inawabebesha dhima ya mashambulio ya aina hiyo waungaji mkono wa ugaidi katika eneo na bwana wao Marekani.