-
Eneo la Puntland la Somalia lapata rais mpya
Jan 08, 2019 21:31Bunge la eneo lenye mamlaka ya ndani la Puntland limemchagua Said Abdullahi Deni kuwa rais eneo hilo, kuchukua nafasi ya Abdiweli Mohamed Ali Gaas.
-
Somalia yakataa ombi la kuangalia upya uamuzi wa kumfukuza mjumbe wa UN
Jan 05, 2019 04:14Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameeleza kusikitishwa kwake na hatua ya kufukuzwa nchini Somalia, Nicholas Haysom, mjumbe maalumu wa umoja huo katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika, lakini amesisitiza kuwa nafasi hiyo itajazwa katika siku chache zijazo.
-
Somaliland yalalamikia hatua ya Somalia kumtimua mjumbe wa UN
Jan 03, 2019 23:20Jamhuri iliyojitangazia uhuru ya Somaliland nchini Somalia imekosoa vikali hatua ya serikali ya Mogadishu ambayo Jumanne iliyopita ilimfukuza nchini humo Nicholas Haysom, mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa, kutokana na kile ilichokitaja kama mienendo yake mibaya na kuingilia kwake waziwazi mambo ya ndani ya nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Somalia yamfukuza mjumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo
Jan 01, 2019 23:40Wizara ya Mambo ya Nje ya Somalia imesema kuwa Nicholas Haysom, mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa hatakiwi nchini humo na imemtaka aondoke haraka Somalia.
-
IFJ: Waandishi habari karibu mia moja wameuawa mwaka 2018 duniani
Jan 01, 2019 23:20Shirikisho la Kimataifa la Waandishi wa Habari (IFJ) limetangaza kuwa, waandishi habari 94 waliuawa mwaka uliomalizika wa 2018 katika maeneo mbalimbali ya dunia.
-
Mratibu wa mashambulizi yaliyoua makumi ya watu Mogadishu auawa Somalia
Dec 24, 2018 10:17Mratibu wa mashambulizi ya kigaidi yaliyoua makumi ya raia na kujeruhi wengine wasiopungua 40 mwaka 2017 mjini Mogadishu ameuawa leo nchini Somalia.
-
Watu 16 wapoteza maisha katika hujuma ya kigaidi Mogadishu, Somalia
Dec 22, 2018 11:45Watu 16 wamepoteza maisha kufuatia hujuma ya kigaidi katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.
-
AU yaitaka Burundi ipunguze askari wake Somalia
Dec 21, 2018 11:13Umoja wa Afrika umeitaka Burundi ipunguze askari wake katika kikosi cha kulinda amani cha umoja huo, maarufu kama AMISOM, nchini Somalia.
-
Magaidi 62 wa Al Shabab waangamizwa Somalia
Dec 18, 2018 03:51Jeshi la Kitaifa la Somalia limetangaza kuwa magaidi 62 wa Al Shabab wameangamizwa katika oparesheni iliyofanyika kwenye eneo la Gandarsh katika jimbo la Banaadir la kusini mwa nchi hiyo.
-
Jeshi la Somalia na AU zafanya operesheni ya pamoja dhidi ya al Shabab
Dec 17, 2018 11:52Mkuu wa mipango ya opereshenei ya kikosi cha Umoja wa Afrika cha kulinda amani Somalia (AMISOM) amesema kuwa, askari wa kikosi hicho na wale wa serikali wanaendesha kwa pamoja operesheni ya kupambana na magaidi wa al Shabab kusini mwa Somalia.