-
Utafiti: Mashambulizi ya anga ya Marekani huko Somalia hayana tija
Nov 11, 2018 10:50Utafiti mpya umesema mashambulizi ya anga yanayofanywa kila uchao na Marekani nchini Somalia yameshindwa kulitokomeza au hata kulidhoofisha kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab na badala yake yamekuwa na taathira hasi kwa raia wa kawaida.
-
Watu zaidi ya 30 wauawa katika mashambulizi ya kigaidi Mogadishu
Nov 09, 2018 23:56Watu zaidi ya 30 wameuawa katika mashambulizi ya kigaidi yaliyolenga Hoteli ya Sahafi mjini Mogadishu ambayo hutumiwa zaidi na maafisa wa serikali ya Somalia.
-
Mbunge auawa katika mripuko wa bomu Mogadishu, Somalia
Nov 08, 2018 12:18Polisi ya Somalia imesema mbunge mmoja wa eneo la HirShabelle amepoteza maisha katika mripuko wa bomu uliotokea adhuhuri ya leo katika mji mkuu wa nchi hiyo, Mogadishu.
-
Mkuu wa fedha wa al-Shabaab ya Somalia auawa
Oct 26, 2018 10:32Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM kimetangaza habari ya kufanikiwa kumuangamiza Mdhibiti Mkuu wa Fedha wa kundi la kigaidi na ukufurishaji la al-Shabaab.
-
Watu zaidi ya 50 wauawa katika mapigano baina ya koo huko Somaliland, Somalia
Oct 24, 2018 13:01Mapigano yaliyojiri kati ya koo hasimu katika kijiji cha Dhumey eneo la Somaliland lililojitenga na Somalia yamesababisha vifo vya watu zaidi ya 50.
-
Idadi ya vifo katika miripuko wa Somalia yaongezeka
Oct 15, 2018 04:21Idadi ya wahanga wa mashambulio mawili ya kujiripua kwa mabomu iliyotokea kusini magharibi mwa Somalia imeongezeka. Taarifa zinasema kuwa watu 20 wamepoteza maisha na wengine 40 wamejeruhiwa katika miripuko hiyo miwili iliyopishana kwa dakika chache tu.
-
Watu 16 wauawa katika shambulizi la kigaidi Somalia
Oct 14, 2018 03:36Kwa akali watu 16 wameuawa katika shambulizi la bomu lililofanywa na kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab katika mji wa Baidoa nchini Somalia.
-
Al-Shabaab ya Somalia yaua 5 kwa tuhuma za ujasusi
Oct 10, 2018 11:19Kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab la Somalia lenye mfungamano na mtandao wa kigaidi wa al-Qaeda limewaua kwa kuwamiminia risasi watu watano kwa tuhuma za kufanya ujasusi kwa niaba ya vyombo vya kiintelejensia vya Marekani, Uingereza na Somalia.
-
Aliyekuwa kamanda wa al-Shabaab anyimwa idhini ya kuwania urais Somalia
Oct 06, 2018 00:20Serikali ya Mogadishu imemnyima kibali cha kugombea urais wa jimbo moja la Somalia, aliyekuwa Naibu Kiongozi wa kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab na pia msemaji wa zamani wa genge hilo la ukufurishaji, Mukhtar Robow Abu Mansur, ambaye mwaka jana alijisalimisha kwa jeshi la nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Al Shabab washambulia msafara wa Umoja wa Ulaya, watu 3 wauawa Mogadishu
Oct 01, 2018 11:07Watu watatu wameuawa katika shambulizi la kujilipua kwa bomu lililofanywa na wanachama wa kundi la kigaidi la al Shabab dhidi ya msafara wa Umoja wa Ulaya mjini Mogadishu.