-
Puntland yatangaza hali ya hatari kutokana na ukame
Dec 06, 2017 04:24Eneo lenye mamlaka ya ndani la Puntland nchini Somalia limetangaza hali ya hatari kutokana na kushtadi ukame, huku likiiomba jamii ya kimataifa msaada wa chakula na maji.
-
AMISOM: Kupunguzwa wanajeshi wa AU Somalia kutakuwa na taathira hasi
Dec 04, 2017 23:43Kikosi cha Askari wa Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM kimeeleza wasi wasi wake kuhusiana na mpango wa kupunguza idadi ya wanajeshi wanaohudumu kwenye kikosi hicho.
-
Idadi ya waliopoteza maisha katika hujuma ya kigaidi Somalia Oktoba yafika 512
Dec 02, 2017 00:45Watu 512 sasa wamebainika kupoteza maisha katika miripuko miwili ya mabomu iliyojiri katika mkuu wa Somalia, Mogadishu mwezi Oktoba, imesema kamati ya kuchunguza hujuma hiyo.
-
Al-Shabaab yadai kuua askari kadhaa wa Somalia, akiwemo kamanda
Dec 03, 2017 23:09Kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh (ISIS) linadai kuwa limeua askari kadhaa wa Jeshi la Ulinzi la Somalia SNA akiwemo kamanda wa ngazi za juu wa jeshi hilo.
-
Waziri wa Masuala ya Dini wa Somalia afutwa kazi
Nov 26, 2017 10:33Hassan Ali Khayre, Waziri Mkuu wa Somalia amemfuta kazi Waziri wa Masuala ya Dini wa nchi hiyo bila kutangaza sababu ya uamuzi wake huo.
-
Wanamgambo wa al Shabab zaidi ya 100 wauawa katika shambulio la Marekani Somalia
Nov 21, 2017 23:35Jeshi la Marekani limeeleza kuwa limeuwa wanamgambo wa kundi la al Shabab zaidi ya 100 katika shambulio la ndege za kivita za nchi hiyo dhidi ya kambi ya kundi hilo huko Somalia.
-
Wananchi wa Somaliland washiriki uchaguzi wa rais, matokeo Ijumaa
Nov 14, 2017 03:53Mamia ya maelfu ya wananchi wa eneo lenye mamlaka ya ndani la Somaliland nchini Somalia wamejitokeza katika uchaguzi wa kumchagua rais wa tano wa eneo hilo, ambao unashuhudia ushindani mkali kati ya serikali na kambi ya upinzani.
-
Marekani imezidisha harakati zake za kijeshi nchini Somalia
Nov 13, 2017 04:40Kamandi ya jeshi la Marekani barani Afrika imetangaza kuwa nchi hiyo imeongeza kiwango cha harakati zake za kijeshi nchini Somalia.
-
Zaidi ya wakimbizi laki moja wamesharejea Somalia
Nov 11, 2017 04:14Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR limetangaza kuwa, zaidi ya wakimbizi laki moja wa Kisomali wamesharejea nchini kwao.
-
AMISOM kuondoa askari 1,000 nchini Somalia licha ya kuendelea kukosekana uthabiti nchini humo
Nov 09, 2017 04:13Ujumbe wa Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) umetangaza kuwa utaondoa askari 1,000 kutoka Somalia kufikia mwishoni mwa mwaka huu.