-
AMISOM kuondoa askari 1,000 nchini Somalia
Nov 08, 2017 11:56Ujumbe wa Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) umetangaza kuwa utaondoa askari 1,000 kutoka Somalia hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu.
-
Jeshi la Somalia lakomboa maeneo muhimu yaliyokuwa chini ya al-Shabaab
Nov 05, 2017 11:36Vikosi vya jeshi la Somalia vimefanikiwa kukomboa ngome nyeti zilizokuwa chini ya makucha ya kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab katika maeneo ya Shabelle ya Chini na Kati.
-
Malengo ya hatua za kijeshi za Marekani nchini Somalia
Nov 04, 2017 23:43Kutokana na kushadidi mashambulizi ya kigaidi katika ardhi ya Somalia, ndege za kivita za Marekani kwa mara ya kwanza zimefanya mashambulizi dhidi ya ngome za makundi ya kigaidi katika nchi hiyo ya mashariki mwa Afrika.
-
Magaidi wa al Shabab wateka mji wa Rassadi kusini mwa Somalia
Nov 01, 2017 04:51Kundi la kigaidi la al Shabab limeuteka mji wa Rassadi ulioko kusini mwa Somalia baada ya askari wa kulinda amani wa Umoja wa Afrika kuondoka katika eneo hilo.
-
Rais wa Somalia atangaza azma imara ya kupambana na ugaidi
Oct 31, 2017 10:12Rais wa Somalia ametangaza azma yake imara ya kupambana na magaidi katika nchi hiyo ambayo wiki za hivi karibuni imepoteza mamia ya watu katika mashambulio ya magaidi.
-
Umoja wa Ulaya wataka kutatuliwa hitilafu za ndani nchini Somalia
Oct 30, 2017 10:09Umoja wa Ulaya umetoa wito wa kupatiwa ufumbuzi hitilafu za ndani nchini Somalia ili kuboresha hali ya usalama wa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika inayokabiliwa na hali ya mchafukoge.
-
Wakuu wa usalama wapigwa kalamu kufuatia mashambulizi ya kigaidi Somalia
Oct 29, 2017 12:29Wakuu wa vyombo vya usalama nchini Somalia wamepigwa kalamu nyekundu kufuatia mashambulizi ya kigaidi ya jana Jumamosi yaliyosababisha makumi ya watu kuuawa na kujeruhiwa.
-
Watu 10 wauawa 16 wajeruhiwa katika shambulizi jipya nchini Somalia
Oct 25, 2017 12:07Mripuko wa bomu la kutegwa ardhini na ufyatulianaji risasi baina ya askari wa AU na wanamgambo wa al Shabab umeua watu wasiopungua 10 na kujeruhi wengine 16 kusini mwa Somalia.
-
Ethiopia kuendelea kushirikiana na Somalia katika vita dhidi ya al-Shabaab
Oct 25, 2017 00:33Waziri Mkuu wa Ethiopia, Hailemariam Desalegn amesema nchi yake itaendelea kushirikiana na Somalia katika mapambano dhidi ya kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab.
-
Watu saba wauawa katika hujuma ya kigaidi karibu na Mogadishu, Somalia
Oct 22, 2017 10:25Watu wasiopungua saba, wengi wakiwa wanawake wakulima, wameuawa karibu na mji mkuu wa Somalia kufuatia hujuma ya kigaidi huku mji huo ukiwa bado unaomboleza shambulizi la hivi karibuni lililoua mamia ya watu.