-
Msalaba Mwekundu: Dunia ina miezi 3 kunusuru mamilioni wanaokabiliwa na njaa Somalia, Yemen
Mar 22, 2017 11:41Shirika la Msalaba Mwekundu limeonya kuwa, jamii ya kimataifa ina miezi mitatu hadi minne kuokosoa maisha ya mamilioni ya watu wanaokabiliwa na baa la njaa katika nchi za Somalia na Yemen.
-
Waziri Mkuu Mpya wa Somalia atangaza baraza jipya la mawaziri 26
Mar 21, 2017 10:48Waziri Mkuu Mpya wa Somalia leo ametangaza baraza lake la mawaziri 26 na kumteua waziri wa zamani wa mambo ya nje kuwa Waziri wa Fedha huku akimteuwa pia mwandishi wa habari wa BBC kuwa mwanadiplomasia wa ngazi ya juu wa nchi hiyo.
-
Waziri Mkuu wa Somalia: Saudia, mhusika wa mauaji ya wakimbizi wa Kisomali
Mar 20, 2017 11:38Serikali ya Somalia imesema kuwa utawala wa Saudi Arabia ndio uliohusika na mauaji ya wakimbizi wa nchi hiyo katika maji ya Yemen.
-
Saudia yaitaka UN isimamie bandari ya Yemen baada ya kuua kikatili Wasomali 44
Mar 20, 2017 04:31Muungano vamizi wa kijeshi wa Saudi Arabia nchini Yemen umeutaka Umoja wa Mataifa uchukue udhibiti wa bandari ya Hudaydah baada ya helikopta ya Aal-Saud aina ya Apache kufanya shambulio la kikatili dhidi ya boti ya wakimbizi karibu na Lango Bahari la Bab al-Mandab, pwani ya Yemen na kuua makumi ya raia wa Somalia.
-
Mkuu wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika aitembelea Somalia
Mar 19, 2017 03:42Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Moussa Faki Mahamat ameongoza ujumbe wa ngazi za juu wa umoja huo katika ziara ya kuitembelea Somalia.
-
UN, IOM zalaani mauaji ya wakimbizi 42 wa Kisomali, pwani ya Yemen
Mar 18, 2017 03:44Shirika la Kimataifa la Wahajiri (IOM) limekosoa vikali shambulio lililoua makumi ya wakimbizi raia wa Somalia katika pwani ya Yemen usiku wa kuamkia jana.
-
Wanamgambo wa al Shabab wauawa kusini mwa Somalia
Mar 17, 2017 23:21Wanamgambo kadhaa wa kundi la kigaidi la al Shabab wameuawa katika oparesheni iliyofanywa na jeshi la Somalia katika maficho ya kundi hilo kusini mwa nchi hiyo
-
Kiongozi mmoja mwandamizi wa al Shabab auawa Somalia
Mar 16, 2017 23:54Maafisa wa ngazi za juu wa masuala ya ulinzi na usalama wa Somalia wametangaza habari ya kuuawa mmoja wa viongozi waandamizi wa genge la kigaidi la al Shabab katika mji mkuu wa nchi hiyo, Mogadishu.
-
Watu 8 wauawa, katika mripuko wa bomu Mogadishu, Somalia
Mar 13, 2017 10:56Polisi ya Mogadishu, mji mkuu wa Somalia imetangaza habari ya kuuawa watu wanane katika mripuko wa bomu uliotokea leo mjini humo.
-
Indhari ya Umoja wa Mataifa ya kutokea maafa ya kutisha zaidi ya hali mbaya ya kibinaadamu
Mar 13, 2017 02:35Kutokana na kuenea ukame na njaa katika maeneo tofauti ya dunia Umoja wa Mataifa umetahadharisha kuhusu hatari ya kutokea maafa makubwa zaidi ya kibinaadamu ambayo hayajawahi kushuhudiwa katika miaka 72 iliyopita