-
Rais wa Tunisia amfuta kazi waziri kwa vifo vya makumi ya Mahujaji Makka
Jun 22, 2024 11:18Rais Kais Saied wa Tunisia amempiga kalamu nyekundu Waziri wa Masuala ya Dini wa nchi hiyo, Brahim Chaibi, akimbebesha dhima ya vifo vya makumi wa raia wa nchi hiyo, waliokuwa miongoni mwa malaki ya Mahujaji wa Nyumba Tukufu ya Allah mjini Makka, Saudi Arabia mwaka huu.
-
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu asisitiza kuendelea ushirikiano kati ya Iran na Qatar
May 23, 2024 05:02Ayatullah Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, katika kikao na "Tamim bin Hamad Al-Thani" Amir wa Qatar na ujumbe aliofuatana nao, ameishukuru Qatar kwa rambirambi zake katika msiba wa kufa shahidi Sayyid Ebrahim Raisi na mashahidi wenzake, na kusisitiza haja ya kuendelea ushirikiano kati ya nchi hizi mbili.
-
Watunisia waandamana kupinga 'uingiliaji wa kigeni'
May 20, 2024 06:54Wananchi wa Tunisia wamefanya maandamano kulaani na kupinga hatua ya nchi za Magharibi ya kuingilia masuala ya ndani ya nchi hiyo.
-
Ofisi ya Haki za Binadamu ya UN yabainisha wasiwasi wake kuhusu kukandamizwa wahamiaji Tunisia
May 18, 2024 07:29Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa jana ilibainisha wasiwasi wake kuhusu "kuongezeka ukandamizaji na vitendo vya mabavu dhidi ya wahamiaji nchini Tunisia. Ofisi hiyo imesema kuwa haki za wahamiaji wote zinapasa kulindwa.
-
Upinzani Tunisia wataka dhamana ya uchaguzi huru na wa haki wa rais
May 13, 2024 06:24Wafuasi wa chama cha Salvation Front wanaompinga Rais Kais Saied wa Tunisia, waliandamana jana Jumapili katikati mwa mji mkuu, Tunis, wakitaka kusafishwa mazingira na hali ya kisiasa, kupangwa tarehe ya uchaguzi wa rais, na kutoa dhamana ya uchaguzi wa kidemokrasia na wa haki kwa wananchi.
-
Iran yatathmini njia za kuimarisha uhusiano wake na Tunisia
May 06, 2024 07:47Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu inachunguza njia na majukwaa ya kuimarisha zaidi uhusiano wa pande mbili kati yake na Tunisia.
-
Watunisia waandamana mbele ya ubalozi wa Marekani mjini Tunis dhidi ya Israel
Mar 12, 2024 07:41Wananchi wa Tunisia jana waliandamana mbele ya ubalozi wa Marekani huko Tunis mji mkuu wa Tunisia kulaani mauaji ya kimbari yanayoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya raia wa Kipalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Ghannouchi, kiongozi wa upinzani Tunisia aliyefungwa jela aanza mgomo wa kususia kula
Feb 20, 2024 07:06Rached Ghannouchi, mwanasiasa mashuhuri wa upinzani nchini Tunisia na kiongozi wa chama cha Ennahda, ameanza mgomo wa kususia kula akiwa kifungoni jela kuonyesha mshikamano na wanaharakati wenzake wanaopinga serikali.
-
Wahajiri 40 wahofiwa kufa maji wakielekea Italia
Jan 17, 2024 07:40Makumi ya wahajiri wanahofiwa kupoteza maisha wakiwa katika safari ya baharini wakielekea Italia.
-
Watunisia wafanya maandamano makubwa mbele ya ubalozi wa Marekani kuiunga mkono Gaza
Dec 25, 2023 02:41Wananchi wa Tunisia jana Jumapili walifanya maandamano mkabala wa ubalozi wa Marekani katika mij mkuu wa nchi hiyo Tunis, kwa ajili ya kuiunga mkono Gaza. Wananchi wa Tunisia wamekuwa wakiandamana kwa ajili ya kuwaunga mkono raia wa Palestina wa Ukanda wa Gaza na kupinga mashambulizi ya kikatili ya utawala wa Kizayuni.