-
Tunisia yaizuia meli ya utawala haramu wa Israel isitie nanga katika bandari yake
Aug 18, 2018 04:14Harakati ya Kimataifa ya Kuususia Utawala Haramu wa Israel, imesema kuwa serikali ya Tunisia ilikataa kuiruhusu meli moja ya utawala huo katili kutia nanga katika bandari ya nchi hiyo.
-
Watunisia waandamana kulalamikia ubaguzi wa Saudia katika kutoa viza kwa ajili ya Hijja
Aug 14, 2018 15:03Raia wa Tunisia wamefanya maandamano kulalamikia siasa za kibaguzi zinazotekelezwa na Saudi Arabia katika kutoa viza kwa ajili ya kushiriki ibada ya Hijja ya mwaka huu.
-
Watunisia waandamana kupinga mageuzi ya kijamii yaliyopendekezwa na kamati ya Rais
Aug 12, 2018 07:54Maelfu ya wananchi wa Tunisia wameandamana kupinga mageuzi ya kijamii yaliyopendekezwa na kamati iliyoundwa na rais wa nchi hiyo Beji Caid Essebsi.
-
Tunisia yakosoa uingiliaji kati wa nchi ajinabi huko Libya
Aug 08, 2018 06:44Waziri wa Mambo ya Nje wa Tunisia ameeleza wasiwasi wake kuhusu hali ya machafuko inayoendelea kushuhudiwa nchini Libya na kusema kuwa nchi hiyo imekuwa medani ya vita vya niaba vya pande za kigeni.
-
Bunge la Tunisia lampigia kura ya kuwa na imani naye Waziri Mpya wa Mambo ya Ndani
Jul 29, 2018 13:55Bunge la Tunisia limepiga kura ya kuwa na imani na Waziri mpya wa Mambo ya Ndani katika kipindi hiki ambacho nchi hiyo inakabiliwa na mgogoro wa kisiasa sambamba na miito ya kuitaka serikali ijiuzulu.
-
Waziri Mkuu wa Tunisia akataa kujiuzulu
Jul 26, 2018 03:05Waziri Mkuu wa Tunisia amekataa ombi la Rais wa nchi hiyo aliyemtaka ajiuzulu.
-
Chama cha Al Nahdha chapinga Youssef Chahed kugombea uchaguzi wa rais
Jul 18, 2018 07:33Chama cha Kiislamu nchini Tunisia cha al Nahadha kimepinga Waziri Mkuu wa nchi hiyo kugombea uchaguzi wa rais nchini humo.
-
Aliyekuwa mlinzi wa Bin Laden atiwa mbaroni nchini Tunisia
Jul 15, 2018 07:16Mlinzi wa aliyekuwa kiongozi wa mtandao wa al Qaida, Usama bin Laden ametiwa mbaroni nchini Tunisia, baada ya kutimuliwa nchini Ujerumani.
-
Tunisia yaanza kusikiliza kesi ya mauaji ya dikteta wa zamani wa nchi hiyo
Jul 14, 2018 08:02Serikali ya Tunisia imeanza kusikiliza kesi dhidi ya dikteta wa zamani wa nchi hiyo, Zine El Abidine Ben Ali, kwa kuhusika na mauaji ya waandamanaji katika vuguvugu lililomuondoa madarakani mwaka 2011.
-
Jeshi la Algeria laanza oparesheni kubwa karibu na mpaka wa Tunisia
Jul 12, 2018 07:31Jeshi la Algeria limeanzisha oparesheni kubwa katika maeneo ya mpaka wa pamoja na nchi jirani ya Tunisia kufuatia kutekelezwa shambulio la kigaidi Jumapili iliyopita katika mkoa mmoja ulioko mpakani wa Jendouba. Wanajeshi sita waliuawa na watatu kujeruhiwa katika shambulio hilo la kigaidi.