Watunisia waandamana kupinga mageuzi ya kijamii yaliyopendekezwa na kamati ya Rais
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i47394-watunisia_waandamana_kupinga_mageuzi_ya_kijamii_yaliyopendekezwa_na_kamati_ya_rais
Maelfu ya wananchi wa Tunisia wameandamana kupinga mageuzi ya kijamii yaliyopendekezwa na kamati iliyoundwa na rais wa nchi hiyo Beji Caid Essebsi.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Aug 12, 2018 03:24 UTC
  • Watunisia waandamana kupinga mageuzi ya kijamii yaliyopendekezwa na kamati ya Rais

Maelfu ya wananchi wa Tunisia wameandamana kupinga mageuzi ya kijamii yaliyopendekezwa na kamati iliyoundwa na rais wa nchi hiyo Beji Caid Essebsi.

Wananchi hao wanaojumuisha watu wa matabaka mbalimbali wakiwemo wasomi wa vyuo vikuu na shakhsia wa dini ya Kiislamu wameandamana kuitikia wito uliotolewa na jopo la "Uratibu wa Kitaifa kwa ajili ya Kulinda Qur'ani na Katiba" na kutangaza upinzani wao dhidi ya mapendekezo hayo ya mageuzi ya kijamii.

Huku wakiwa na misahafu mikononi mwao, waandamanaji hao wamesisitiza kuwa wataulinda na kuuhami Uislamu kwa damu zao.

Rais Beji Caid Essebsi wa Tunisia

Kutokana na kampeni ya uhuru wa mtu binafsi inayoendeshwa nchini Tunisia, kamati iliyoundwa na rais wa nchi hiyo mwaka uliopita wa 2017 iliwasilisha mapendekezo makubwa ya kijamii ambayo hayajawahi kushuhudiwa yakiwemo ya kutaka mirathi itolewe kwa usawa kati ya mwanamke na mwanamme, kuondolewa hukumu ya kuwa kosa la jinai maingiliano ya kimwili ya watu wa jinsia moja na vile vile kufutwa hukumu ya adhabu ya kifo.../