• Afya ya kiongozi mkongwe wa upinzani nchini Uganda aliyeko gerezani yadaiwa kuzorota

    Afya ya kiongozi mkongwe wa upinzani nchini Uganda aliyeko gerezani yadaiwa kuzorota

    Jan 21, 2026 02:39

    Chama cha upinzani nchini Uganda cha People’s Front for Freedom kimesema katika taarifa kwamba afya ya kiongozi mkongwe wa upinzani nchini humo Kizza Besigye “iko katika hali mbaya na inaendelea kudhoofika,” na kutoa mwito wa kutaka aruhusiwe kukaguliwa na madaktari wake binafsi pamoja na familia yake.

  • Uchaguzi Uganda; Bobi Wine apinga ushindi wa Museveni

    Uchaguzi Uganda; Bobi Wine apinga ushindi wa Museveni

    Jan 18, 2026 10:26

    Kiongozi wa upinzani na mshindani mkuu wa Rais Yoweri Museveni katika uchaguzi mkuu wa hivi karibuni nchini Uganda, Robert Kyangulani maarufu kama Bobi Wine amesema hakubaliani na matokeo ya uchaguzi wa rais yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi ya nchi hiyo.

  • Tume ya Uchaguzi Uganda: Museveni aongoza kwa asilimia 61.7 ya kura

    Tume ya Uchaguzi Uganda: Museveni aongoza kwa asilimia 61.7 ya kura

    Jan 16, 2026 07:14

    Matokeo ya awali yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi ya Uganda yanaonyesha kuwa Rais Museveni ameibuka na asilimia 61.7 ya kura halali zilizohesabiwa hadi sasa.

  • Zoezi la kuhesabu kura nchini Uganda linaendelea

    Zoezi la kuhesabu kura nchini Uganda linaendelea

    Jan 15, 2026 15:11

    Shughuli za kuhesabu kura zimeanza katika vituo mbalimbali vya kupigia kura kote Kampala na sehemu zingine za Uganda, baada ya kumalizika kwa zoezi la upigaji kura.

  • Bobi Wine: Nitapitia upya mikataba ya mafuta ya Uganda iwapo nitachaguliwa Rais

    Bobi Wine: Nitapitia upya mikataba ya mafuta ya Uganda iwapo nitachaguliwa Rais

    Jan 08, 2026 12:48

    Bobi Wine mgombea mkuu wa upinzani katika uchaguzi wa kiti cha urais nchini Uganda uliopangwa kufanyika wiki ijayo, amesema kuwa atapitia upya makubaliano yaliyofikiwa kati ya nchi hiyo na makampuni ya mafuta duniani iwapo ataibuka na ushindi. Amesema ataifanyia marekebisho mikataba yoyote ambayo haina manufaa na maslahi kwa watu wa Uganda.

  • Mgombea urais Uganda: Nilipigwa na askari usalama

    Mgombea urais Uganda: Nilipigwa na askari usalama

    Dec 07, 2025 12:19

    Bob Wine au Robert Kyagulanya mgombea kiti cha urais nchini Uganda kwa tiketi ya chama cha upinzani cha NUP amesema kuwa askari usalama wa nchi hiyo wampiga yeye na wafuasi wake wakati walipokuwa katika kampeni za uchaguzi kaskazini mwa nchi hiyo katika kile kinachotajwa kuwa muendelezo wa ghasia na utumiaji mabavu unaoshuhudiwa Uganda kabla ya uchaguzi wa Rais Januari 15 mwakani.

  • Uchaguzi Uganda: UN yalaani ukandamizaji dhidi ya mgombea urais wa upinzani

    Uchaguzi Uganda: UN yalaani ukandamizaji dhidi ya mgombea urais wa upinzani

    Dec 04, 2025 03:47

    Umoja wa Mataifa jana Jumatano ulikosoa kuongezeka ukandamizaji dhidi ya upinzani na vyombo vya habari nchini Uganda kabla ya uchaguzi mkuu wa mwezi ujao, na kutaka uchunguzi ufanyike bila upendeleo kuhusu madai ya kukamatwa raia kiholela, kutoweka na "mateso".

  • Mahakama ya ICC yathibitisha mashtaka dhidi ya Joseph Kony

    Mahakama ya ICC yathibitisha mashtaka dhidi ya Joseph Kony

    Nov 08, 2025 04:10

    Majaji katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC yenye makao yake mjini Hague, Uholanzi wamethibitisha kuwa kiongozi wa waasi wa Uganda Joseph Kony anakabiliwa na mashtaka ya jinai za kivita na jinai dhidi ya binadamu na hivyo kufungua njia kwa ajili kuanza kesi yake iwapo tu atatiwa nguvuni.

  • Watu 46 wamefariki dunia katika ajali mbaya ya barabarani  Uganda

    Watu 46 wamefariki dunia katika ajali mbaya ya barabarani Uganda

    Oct 22, 2025 12:57

    Polisi ya Uganda imeripoti kuwa watu 46 wamepoteza maisha na wengine kadhaa kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha mabasi mawili katika barabara kuu ya Kampala kuelekea Gulu nchini humo mapema leo Jumatano.

  • Araghchi kuhudhuria mkutano wa NAM nchini Uganda

    Araghchi kuhudhuria mkutano wa NAM nchini Uganda

    Oct 15, 2025 02:34

    Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu, Abbas Araghchi atazuru Uganda karibuni hivi kushiriki Mkutano wa 19 wa Mawaziri wa Jumuiya ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote (NAM).