-
Mwana wa Rais wa Uganda amuita 'Hitler' kiongozi wa RSF aliyekutana na baba yake hivi karibuni
Feb 24, 2026 07:43Mwana mtatanishi wa Rais wa Uganda Yoweri Museveni ambaye ni mkuu wa majeshi ya nchi hiyo Muhoozi Kainerugaba ametoa matamshi yasiyo ya kawaida katika kumshambulia kiongozi wa wanamgambo wa Sudan wa Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF), Mohamed Hamdan Dagalo ambaye hivi karibuni alikutana na baba yake huko nchini Uganda.
-
Afya ya kiongozi mkongwe wa upinzani nchini Uganda aliyeko gerezani yadaiwa kuzorota
Jan 20, 2026 23:09Chama cha upinzani nchini Uganda cha People’s Front for Freedom kimesema katika taarifa kwamba afya ya kiongozi mkongwe wa upinzani nchini humo Kizza Besigye “iko katika hali mbaya na inaendelea kudhoofika,” na kutoa mwito wa kutaka aruhusiwe kukaguliwa na madaktari wake binafsi pamoja na familia yake.
-
Uchaguzi Uganda; Bobi Wine apinga ushindi wa Museveni
Jan 18, 2026 06:56Kiongozi wa upinzani na mshindani mkuu wa Rais Yoweri Museveni katika uchaguzi mkuu wa hivi karibuni nchini Uganda, Robert Kyangulani maarufu kama Bobi Wine amesema hakubaliani na matokeo ya uchaguzi wa rais yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi ya nchi hiyo.
-
Tume ya Uchaguzi Uganda: Museveni aongoza kwa asilimia 61.7 ya kura
Jan 16, 2026 03:44Matokeo ya awali yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi ya Uganda yanaonyesha kuwa Rais Museveni ameibuka na asilimia 61.7 ya kura halali zilizohesabiwa hadi sasa.
-
Zoezi la kuhesabu kura nchini Uganda linaendelea
Jan 15, 2026 11:41Shughuli za kuhesabu kura zimeanza katika vituo mbalimbali vya kupigia kura kote Kampala na sehemu zingine za Uganda, baada ya kumalizika kwa zoezi la upigaji kura.
-
Bobi Wine: Nitapitia upya mikataba ya mafuta ya Uganda iwapo nitachaguliwa Rais
Jan 08, 2026 09:18Bobi Wine mgombea mkuu wa upinzani katika uchaguzi wa kiti cha urais nchini Uganda uliopangwa kufanyika wiki ijayo, amesema kuwa atapitia upya makubaliano yaliyofikiwa kati ya nchi hiyo na makampuni ya mafuta duniani iwapo ataibuka na ushindi. Amesema ataifanyia marekebisho mikataba yoyote ambayo haina manufaa na maslahi kwa watu wa Uganda.
-
Mgombea urais Uganda: Nilipigwa na askari usalama
Dec 07, 2025 08:49Bob Wine au Robert Kyagulanya mgombea kiti cha urais nchini Uganda kwa tiketi ya chama cha upinzani cha NUP amesema kuwa askari usalama wa nchi hiyo wampiga yeye na wafuasi wake wakati walipokuwa katika kampeni za uchaguzi kaskazini mwa nchi hiyo katika kile kinachotajwa kuwa muendelezo wa ghasia na utumiaji mabavu unaoshuhudiwa Uganda kabla ya uchaguzi wa Rais Januari 15 mwakani.
-
Uchaguzi Uganda: UN yalaani ukandamizaji dhidi ya mgombea urais wa upinzani
Dec 04, 2025 00:17Umoja wa Mataifa jana Jumatano ulikosoa kuongezeka ukandamizaji dhidi ya upinzani na vyombo vya habari nchini Uganda kabla ya uchaguzi mkuu wa mwezi ujao, na kutaka uchunguzi ufanyike bila upendeleo kuhusu madai ya kukamatwa raia kiholela, kutoweka na "mateso".
-
Mahakama ya ICC yathibitisha mashtaka dhidi ya Joseph Kony
Nov 08, 2025 00:40Majaji katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC yenye makao yake mjini Hague, Uholanzi wamethibitisha kuwa kiongozi wa waasi wa Uganda Joseph Kony anakabiliwa na mashtaka ya jinai za kivita na jinai dhidi ya binadamu na hivyo kufungua njia kwa ajili kuanza kesi yake iwapo tu atatiwa nguvuni.
-
Watu 46 wamefariki dunia katika ajali mbaya ya barabarani Uganda
Oct 22, 2025 09:27Polisi ya Uganda imeripoti kuwa watu 46 wamepoteza maisha na wengine kadhaa kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha mabasi mawili katika barabara kuu ya Kampala kuelekea Gulu nchini humo mapema leo Jumatano.