China imepinga na kukosoa vikali hatua ya Umoja wa Ulaya ya kuiwekea Jamhuri ya Kiislamu ya Iran vikwazo ilivyovitaja kuwa haramu na vya upande mmoja.
Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya, Josep Borrell amekiri katika mahojiano yake siku ya Alhamisi iliyopita kwamba tunaishi katika ulimwengu wa kambi kadhaa na kwamba kipindi cha udhibiti wa upande mmoja wa Marekani kimefikia tamati.
Waziri wa Masuala ya Nishati wa Qatar ametangaza kuwa haitazamiwi katika msimu ujao wa baridi kali shehena ya gesi iliyopangwa kwenda Asia kuelekea Ulaya.
Shirika la Afya Duniani (WHO) na Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa Ulaya (ECDC) zimeonya kuhusu ongezeko la maambukizi ya ugonjwa wa COVID-19 katika nchi za Ulaya, katika kile kilichotajwa ni wimbi jipya la msambao wa maradhi hayo barani humo.
Shirika la Kimataifa la Nishati IEA limetangaza kwamba kufuatia uamuzi wa Russia wa kusitisha mauzo yake mengi ya gesi kwa Ulaya, bara hilo litakabiliwa na "hatari kubwa isiyo na kifani" ya uhaba wa gesi asilia katika msimu ujao wa baridi kali.
Katika muendelezo wa ubaguzi dhidi ya Waislamu wanaoishi nchini Uingereza, vyombo vya habari vimeripoti wiki hii juu ya kuweko mpango wa kupokonywa uraia wa nchi hiyo Waislamu wanaoishi nchini Uingereza na kutangazwa kuwa raia wa daraja la pili.
Miji kadhaa ya nchi za Ulaya imeshuhudia maandamano ya kulalamikia ongezeko la bei za nishati, huku mgogoro wa mafuta ya petroli na gesi ukiendelea kuyasumbua mataifa mengi ya bara Ulaya.
Mwanasiasa wa mrengo wa kushoto nchini Ujerumani ameikosoa vikali serikali ya nchi hiyo kwa kusababisha alichokiita vita 'vibaya' vya kiuchumi dhidi ya Russia.
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu imehifadhi hisa yake katika soko la nishati licha ya vikwazo, lakini inaweza kuwa na mchango mkubwa katika kupatia suluhu mgogoro wa niashati unaolikabili bara Ulaya.
Mawaziri wa fedha wa nchi saba zilizoendelea kiviwanda duniani, zinazojulikana kama G7, walikubaliana Ijumaa, Septemba 2, katika mkutano uliofanyika kwa njia ya video, kuweka mipaka ya bei kwa mauzo ya mafuta ya Russia.