-
Zarif na Guterres wajadili hali ya Waislamu Warohingya nchini Myanmar
Feb 18, 2017 23:13Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wamejadili na kubadilishana mawazo kuhusu hali mbaya waliyonayo Waislamu wa jamii ya Rohingya nchini Myanmar, hali ya mambo katika nchi za Yemen, Syria na Iraq na nafasi ya Umoja wa Mataifa katika kutatua migogoro hiyo.
-
Katibu Mkuu wa UN: Bila ya njia jumuishi za kisiasa haitowezekana kuishinda Daesh
Feb 18, 2017 12:49Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesisitiza kuwa haitowezekana kulishinda kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh (ISIS) katika nchi za Syria na Iraq pasina kuwa na njia ya ufumbuzi wa kisiasa jumuishi na wa pande zote.
-
UN yasisitiza udharura wa kuundwa nchi huru ya Palestina
Feb 16, 2017 12:25Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesisitiza udharura wa kuundwa nchi huru ya Palestina.
-
UN yaeleza wasiwasi wake kuhusu hali mbaya ya Sudan Kusini
Feb 14, 2017 09:39Umoja wa Mataifa umetahadharisha kuhusu machafuko na mapigano yanayoshadidi zaidi nchini Sudan Kusini.
-
Umoja wa Mataifa wampongeza Rais mpya wa Somalia
Feb 10, 2017 04:44Antonio Guterres, Katibu Mkuu mpya wa Umoja wa Mataifa amempongeza Rais mpya wa Somalia na kumtaka aunde baraza la mawaziri jumuishi.
-
UN na AU zamuunga mkono rais mpya wa Somalia
Feb 10, 2017 00:57Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa zimetangaza uungaji mkono wao kwa rais mpya wa Somalia.
-
UN yatahadharisha juu ya hali mbaya ya kibinaadamu katika mkoa wa Tanganyika Kongo DR
Feb 09, 2017 13:08Umoja wa Mataifa umetahadharisha juu ya hali mbaya ya kibinaadamu katika mkoa wa Tanganyika, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
UN: Zaidi ya Waislamu 1000 wameuawa katika operesheni za jeshi la Myanmar
Feb 09, 2017 12:40Maafisa wawili wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa wamesema kuwa, zaidi ya Waislamu 1000 wa kabila la Rohingya wameuawa katika operesheni za jeshi la Myanmar kaskazini mwa nchi hiyo.
-
UN: Wakimbizi 52,000 wa Sudan Kusini wameingia Uganda mwezi jana
Feb 09, 2017 03:56Umoja wa Mataifa umesema wakimbizi 52,000 raia wa Sudan Kusini waliingia nchini Uganda mwezi uliopita pekee wa Januari, kutokana na kuendelea kushuhudiwa mauaji na machafuko katika nchi yao.
-
Umoja wa Mataifa: Watetezi wa haki za binadamu wanakandamizwa nchini Burundi
Feb 09, 2017 00:58Umoja wa Mataifa umetahadharisha kuhusiana na vitendo vya ukandamizaji dhidi ya watetezi wa haki za binadamu huko nchini Burundi.