-
Umoja wa Mataifa kuimarisha kikosi chake cha kusimamia amani CAR
Oct 01, 2016 12:12Mkurugenzi wa Masuala ya Mawasiliano ya Wasimamia Amani wa Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Afrika ya Kati ametangaza kuwa, umoja huo una mpango wa kuimarisha zaidi kikosi chake katika nchi hiyo.
-
Umoja wa Mataifa: Maefu ya watoto Nigeria wanakabiliwa na hatari ya kifo kutokana na ukame
Oct 01, 2016 10:29Umoja wa Mataifa umetahadharisha kwamba, endapo misaada ya kimataifa haitafika kwa wakati, basi maelfu ya watoto wa kaskazinu mashariki mwa Nigeria watafariki dunia ifikapo mwakani kutokana na ukame na lishe duni.
-
UN: Watoto 75 elfu wapo katika hatari ya kufa njaa Nigeria
Sep 29, 2016 10:24Umoja wa Mataifa umetahadharisha kuwa, maelfu ya watoto wadogo wapo katika hatari ya kupoteza maisha katika kipindi cha mwaka mmoja ujao, kutokana na njaa na utapiamlo 'uliosababishwa' na kundi la wanamgambo wa Boko Haram.
-
UNHCR yataka uchunguzi ufanyike kuhusu machafuko ya Kinshasa
Sep 28, 2016 03:45Umoja wa Mataifa umetaka kufanyike uchunguzi kuhusu ghasia na machafuko yaliyotokea hivi karibuni huko Kinshasa mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
UN yatahadharisha kuhusu hatari ya mauaji ya kimbari Burundi
Sep 21, 2016 10:38Kundi la wachunguzi wa Umoja wa Mataifa limetahadharisha kuhusu hatari ya mauaji ya kimbari yanayonukia huko Burundi na kueleza kuwa, mwenendo jumla wa kauli zenye kuleta mgawanyiko wa kikabila zinazotolewa na serikali ya nchi hiyo zinamaanisha kuwa mzozo unaweza kuenea hadi katika nchi nyingine za Kiafrika.
-
Wasiwasi wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya wakimbizi katika Bonde la Ziwa Chad
Sep 16, 2016 22:12Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limetangaza kuwa kuna ulazima wa kuongezwa misaada kwa ajili ya wakaazi wa eneo la Bonde la Ziwa Chad.
-
UN yatahadharisha kuhusu kushindwa kusoma watoto wakimbizi
Sep 15, 2016 11:55Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) limetahadharisha kuhusu kushindwa kwenda shule watoto wakimbizi.
-
Kufichuliwa jinai mpya za Israel dhidi ya watoto
Sep 14, 2016 03:38Ripoti iliyochapishwa na Shirika la Biashara na Maendeleo la Umoja wa Mataifa kuhusu jinai za utawala wa Kizayuni zimewakasirisha viongozi wa utawala huo.
-
Umoja wa Mataifa watiwa wasiwasi na hali ya Sahara Magharibi
Sep 08, 2016 03:29Umoja wa Mataifa umesema unatiwa wasiwasi na hali ya mambo katika eneo la kusini ya Sahara Magharibi.
-
Ki-moon asisitiza kulindwa umoja wa kisiasa Kongo
Sep 07, 2016 09:25Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameyatolea wito makundi yanayozozana nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kulinda umoja wa kisiasa na kujiunga na mchakato wa mazungumzo ya kitaifa ili nchi hiyo irejee katika hali ya amani na utulivu.