-
Somalia yaitaka UN iiondolee vikwazo vya silaha
Sep 30, 2018 10:35Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Somalia ameutaka Umoja wa Mataifa kuondoa vikwazo vya muda mrefu vya silaha dhidi ya nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Algeria: Afrika imedhulumika katika Umoja wa Mataifa
Sep 30, 2018 04:14Waziri wa Mambo ya Nje wa Algeria amesema, Afrika imedhulumika katika Umoja wa Mataifa na kwenye Baraza la Usalama la umoja huo na kwa hivyo dhulma hiyo inapasa iondolewe.
-
Sudan Kusini yaiambia UN kuwa makubaliano ya amani hayatakiukwa
Sep 29, 2018 04:46Makamu wa Rais wa Sudan Kusini ameuambia mkutano wa 73 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwamba makubaliano ya amani ya mara hii yaliyofikiwa hivi karibuni na mahasimu wa kisiasa wa nchi hiyo changa zaidi barani Afrika yatadumu na wana wingi wa matumaini kwamba hayatakiukwa.
-
Kamisheni ya uchunguzi ya Umoja wa Mataifa kuhusu Burundi yaongezewa muda
Sep 28, 2018 11:03Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa limeiongezea muda wa mwaka mmoja mwingine kamisheni ya uchunguzi ya umoja huo kuhusu hali ya haki za binadamu nchini Burundi.
-
Rais Rouhani afanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa UN; wajadili JCPOA, Syria na Yemen
Sep 27, 2018 01:00Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wamefanya mazungumzo mjini New York ambapo wamejadili masuala mbalimbali yakiwemo makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, mgogoro wa Syria na vita vya Yemen.
-
Amir wa Qatar: Hitilafu zimelilemaza Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi
Sep 26, 2018 04:45Akizungumza jana usiku katika Mkutano wa 73 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa huko New York, Amir wa Qatar amekosoa vikwazo vya Saudi Arabia na waitifaki wake dhidi ya nchi yake na kusema hitilafu zilizopo zimelilemaza Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi.
-
Umoja wa Mataifa walaani shambulizi la kigaidi la Ahvaz Iran
Sep 23, 2018 04:20Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres amelaani shambulio la kigaidi lililoua makumi ya watu kusini magharibi mwa Iran.
-
UN: Ghaza inakaribia kusambaratika kikamilifu, Israel inaendelea kukaidi maamuzi ya kimataifa
Sep 21, 2018 09:36Mratibu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Mashariki ya Kati amekiambia kikao cha Baraza la Usalama la umoja huo kwamba eneo la Ukanda wa Ghaza huko Palestina linakaribia kusambaratika kikamilifu.
-
UNICEF: Katika kila sekunde tano, mtoto mmoja hufariki dunia
Sep 18, 2018 02:55Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa Unicef umesema watoto milioni 6.3 waliaga dunia kabla ya kufikisha miaka 15 mwaka jana 2017, huku nusu ya vifo hivyo vikiripotiwa katika eneo la chini ya Jangwa la Sahara barani Afrika.
-
UN yaelezea kusikitishwa na hali mbaya ya Ukanda wa Ghaza
Sep 16, 2018 21:52Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na masuala ya maendeleo na biashara ametoa ripoti maalumu kuhusu maafa ya kibinadamu ya Ukanda wa Ghaza na kuongezeka kupindukia idadi ya Wapalestina wasio na kazi akisema kuwa hali hiyo inasikitisha sana.