-
Majibu ya Kiongozi Muadhamu kwa barua ya Haniya: Iran haitasita kufanya kila juhudi ili kuzima shari ya utawala wa Kizayuni
Jul 06, 2020 06:52Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran itaendelea kuwasaidia na kuwaunga mkono wananchi madhulumu wa Palestina na kuvunja shari za utawala bandia na ghasibu wa Kizayuni.
-
Maelfu waandamana Israel wakitaka Netanyahu ajiuzulu; anatuhumiwa kufanya ufisadi
Jul 05, 2020 06:22Maelfu ya watu wamefanya maandamano katika miji mbalimbali ya Israel wakimtaka Waziri Mkuu wa utawala huo haramu, Benjamin Netanyahu ajiuzulu kwa tuhuma za kufanya ufisadi na ubadhirifu wa mali ya umma.
-
Spika wa Bunge la Kuwait ataka nchi za Kiarabu zikabiliane na Israel
Jul 04, 2020 23:16Spika wa Bunge la Kuwait ametaka nchi za Kiarabu zichukue hatua kali za kukabiliana na njama za utawala wa Kizayuni wa Israel za kuteka maeneo zaidi ya Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Msemaji wa Hamas: njia pekee ya kuwafukuza Wazayuni ni muqawama
Jul 02, 2020 02:14Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) amesema kuwa njia pekee ya kuwarejsha nyuma Wazayuni ni kuendeleza mapambano na kuongeza kuwa: Maandamano yanayofanywa na wananchi wa Palestina katika maeneo mbalimbali yametuma ujumbe kwamba wataendeleza muqawama na mapambano hadi kupatikane ushindi.
-
HAMAS yatoa onyo kali kwa utawala wa Kizayuni wa Israel
Jun 27, 2020 07:15Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imesisitiza kuwa, mashambulizi ya utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Ghaza yatazidi kuufanya muqawama ushikilie msimamo wake wa kupinga njama za Israel za kuteka ardhi zaidi za Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Ndege za kivita za utawala wa Kizayuni zashambulia Ukanda wa Ghaza
Jun 27, 2020 03:49Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limeetekeleza mashambulizi katika Ukanda wa Gaza usiku wa kuamkia leo Jumamosi.
-
Spika wa Iran: Utawala wa Kizayuni wa Israel unasambaratika kwa ndani
Jun 24, 2020 22:08Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amesema kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel umo katika hali ya kusambaratika kutokea ndani.
-
Kushadidi hitilafu ndani ya baraza la mawaziri la Israel juu ya kadhia ya Ukingo wa Magharibi
Jun 23, 2020 03:15Hitilafu za kimitazamo baina ya Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel, Benjamin Netanyahu na Waziri wa Vita wa utawala huo, Benny Gantz kuhusu mpango wa kulitwaa eneo la Palestina la Ukingo wa Magharibi na kuliunganisha na ardhi nyingine zilighusubiwa zimezizidi kupamba moto huku Netanyahu akimtishia Gantz kuwa atalivunja baraza la mawaziri na kuitisha uchaguzi wa nne wa bunge katika kipindi cha mwaka mmoja.
-
Hizbullah yautahadharisha utawala wa Kizayuni wa Israel, yasema makombora yake yako ange
Jun 21, 2020 23:30Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imeutahadharisha utawala wa kizayuni kwamba iwapo utashambulia ardhi ya Lebanon itashambulia maeneo mbalimbali ya utawala huo kwa kutumia makombora yanayolenga shabaha kwa umakini mkubwa.
-
Wanaharakati wa masuala ya kiraia watoa wito wa kususiwa Israel kimataifa
Jun 20, 2020 22:44Jumuiya ya Kimataifa ya Mshikamano wa Kusini nchini Afrika Kusini imetoa wito wa kususiwa utawala haramu wa Israel katika nyanja za kimataifa.