-
Erdogan: Uturuki inataka kuwa na uhusiano mzuri zaidi na Israel
Dec 26, 2020 02:42Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki amesema nchi yake ingependa iwe na uhusiano mzuri zaidi na Israel na kwamba mazungumzo yanaendelea baina ya pande mbili katika ngazi ya intelijensia.
-
Uturuki yamteua balozi mpya wa Israel baada ya miaka 2
Dec 14, 2020 12:18Uturuki imemteua balozi wake mpya wa Tel Aviv, zaidi ya miaka miwili baada ya Ankara kumuita nyumbani balozi wake aliyekuweko katika utawala haramu wa Israel.
-
Uturuki yakosoa mpango wa nchi za Kiarabu wa kufungua balozi zao Baitul Muqaddas
Nov 28, 2020 08:07Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Mevlut Cavusoglu amesema mpango wa nchi za Kiarabu wa kufungua balozi zao katika mji wa Baitul Muqaddas, utadhoofisha uwezekano wa kuundwa nchi ya Palestina.
-
Ghalibaf: Vikwazo vya Marekani dhidi ya nchi huru, ni siasa zilizofeli
Nov 24, 2020 02:24Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa, vikwazo vya Marekani dhidi ya nchi huru duniani ni siasa zilizofeli na kuongeza kuwa, vikwazo hivyo vimeimarisha misingi ya uchumi wa kutengemea uwezo wa ndani, nchini Iran.
-
Mambo yasiyo na uwazi katika mpango wa amani wa Russia kuhusu mgogoro wa Karabakh
Nov 16, 2020 10:19Mambo ya kutiliwa shaka na yasiyofahamika vizuri katika mkataba wa amani wa Russia kuhusu mgogoro wa Azerbaijan na Armenia juu ya eneo la Nagorno Karabakh, yamenyamaziwa kimya na viongozi wa Azerbaijan na Uturuki.
-
Baada ya kuzingirwa kila upande, wanajeshi wa Uturuki waondoka kwenye kambi nyingine nchini Syria
Nov 08, 2020 11:28Duru mbalimbali za habari zimetangaza kuwa, wanajeshi wa Uturuki wameondoka katika kambi nyingine ya viunga vya kusini mwa mji wa Idlib wa magharibi mwa Syria na kukimbilia katika maeneo mengine yanayodhibitiwa na waasi wa nchi hiyo.
-
Onyo la Lavrov kuhusu uwepo wa mamluki 2000 wa kitakfiri huko Karabakh
Nov 05, 2020 03:58Russia daima imekuwa ikitahadharisha kuhusu hatari ya uwepo wa makundi ya kigaidi yenye misimamo ya kupindukia mpaka katika nchi hiyo na nchi nyingine za Caucasia na Asia ya Kati na kusisitiza udharura wa kupambana na makundi hayo.
-
Erdogan: Dunia ipige vita uadui dhidi ya Uislamu sawa ilivyo katika suala la kupiga vita Uyahudi
Nov 03, 2020 02:45Rais Recep Tayyip Erdoğan wa Uturuki ameitaka dunia ijifunze na kupata somo na ibra kutokana na uzembe wa jamii ya kimataifa iliyoacha kuzuia mauaji ya kimbari ya Waislamu wa Bosnia Herzegovina na kusisitiza kuwa, dunia inapaswa kupiga marufuku na kupambana na chuki na uhasama dhidi ya Uislamu kama ilivyopambana na chuki dhidi ya Uyahudi baada ya Holocaust (yanayodaiwa kuwa mauaji ya Mayahudi wakati wa Vita vya Pili vya Dunia).
-
Waliouawa katika zilzala ya Izmir, Uturuki wapindukia 50
Nov 02, 2020 04:29Idadi ya watu waliopoteza maisha kwenye maafa ya tetemeko la ardhi lililotokea mjini Izmir nchini Uturuki imeripotiwa kufika 51, huku timu za uokoaji zikiendelea kutafuta manusura na maiti zilizokwama chini ya vifusi vya nyumba na majengo yaliyobomolewa na zilzala hiyo.
-
Radiamali ya kindumakuwili ya Ufaransa kufuatia malalamiko ya Waislamu duniani
Oct 28, 2020 07:41Waislamu duniani kote wamekasirishwa na kushadidi vitendo vya chuki dhidi ya Uislamu nchini Ufaransa hasa cha kuchapishwa tena katuni zinazomvunjia heshima Mtume Muhammad SAW. Hasira za Waislamu zimeongezeka maradufu baada ya Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa kutetea vitendo hivyo vya chuki dhidi ya Uislamu kwa kisingizo cha uhuru wa maoni.