Jan 02, 2017 07:06
Katika hali ambayo, Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria amesema katika ujumbe wake kwa mnasaba wa mwaka mpya wa 2017 kwamba, ameazimia kuchukua hatua za kurejesha usalama na uthabiti wa nchi hiyo na wa kieneo, kwa mara nyingine tena kundi la kigaidi la Boko Haram limetishia kutekeleza operesheni za kigaidi katika nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika.