Waasi wa kundi linalopigania kujitenga eneo la Cabinda nchini Angola (FLEC) wamedai kwamba wameua askari 18 wa nchi hiyo.
Duru za kijeshi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zimearifu kukombolewa vijiji vinne kaskazini mashariki mwa nchi hiyo vilivyokuwa vimetekwa na waasi.
Duru za kuaminika nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo zimearifu kuwa baadhi ya waasi wa kundi la Mai-Mai wamekubali kusitisha mashambulizi ikatika eneo la Masisi mkoani Kivu ya Kaskazini.
Waasi wa kundi la FLEC linalopigania kujitenga eneo la Cabinda huko Angola wamedai kuwa wameua wanajeshi wa serikali wasiopungua 12 katika eneo tajiri kwa mafuta kusini mwa nchi hiyo.
Watu wawili wameuawa kwenye mapigano kati ya waasi na vikosi vya jeshi la Kongo katika eneo la Walikale nchini humo.
Mahakama ya kijeshi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imewatuhumu wanachama sita wa kundi la waasi wa Uganda kwa kushiriki katika mauaji wiki iliyopita, ambapo makumi ya raia waliuliwa mashariki mwa Kongo.
Msemaji wa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amesema kuwa makumi ya waasi wa Uganda wamekamatwa mashariki mwa Kongo.
Kwa akali watu watano wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika mapigano makali yaliyojiri kati kati ya Mali, huku duru za kiusalama zikiarifu kuwa askari watano wa serikali wametoweka baada ya kujiri mapigano hayo.
Watu 19 wameuawa katika makabiliano makali kati ya askari wa jeshi la serikali na kundi la wabeba silaha katika jimbo la Niger nchini Nigeria.
Rais Yoweri Museveni wa Uganda ameahidi kuwa serikali yake itaisaidia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kukabiliana na kundi la waasi la ADF-Nalu ambalo limekuwa tishio la muda mrefu la nchi mbili hizo jirani.