-
Ukosoaji wa UN kwa serikali ya Ufaransa kwa kuamiliana vibaya na Waislamu wa nchi hiyo
May 29, 2018 08:17Umoja wa Mataifa umeikosoa serikali ya Ufaransa kwa namna inavyoamiliana na Waislamu na inavyokabiliana na ugaidi na athari za hatua zake hizo ambazo zinatia wasiwasi kwa kutishia uhuru wa mtu binafsi.
-
Wafungwa Waislamu Marekani wanyimwa chakula, walazimishwa kula nyama ya nguruwe
May 24, 2018 14:38Baraza la Mahusiano ya Kiislamu Marekani (CAIR) limewasilisha faili la kesi mahakamani kuwashtaki maafisa wa Idara ya Magereza ya Alaska, kwa kuwanyima chakula wafungwa Waislamu mbali na kuwalazimisha kula nyama ya nguruwe katika mwezi huu wa Ramadhani.
-
Waziri wa Uhajiri wa Denmark atoa matamshi ya kuuvunjia heshima mwezi mtukufu wa Ramadhani
May 22, 2018 08:01Waziri wa Uhajiri, Mshikamano na Maskani wa Denmark ametoa matamshi ya chuki na uadui dhidi ya Uislamu kwa kuwataka Waislamu wa nchi hiyo wanapoanza kufunga na katika kipindi chote cha mwezi mtukufu wa Ramadhani wachukue likizo makazini akidai kwamba amali za mwezi huo ni "hatari" kwa watu wote nchini humo.
-
Waislamu, Wakristo Uganda walalamikia kutozwa ushuru Misahafu, Biblia
May 15, 2018 14:14Viongozi wa kidini nchini Uganda wamekosoa vikali hatua ya Mamlaka ya Kukusanya Ushuru nchini humo URA kuanza kutoza ushuru wa forodha suhula za kidini zinazoingizwa nchini humo kama nakala za Qurani na Biblia.
-
Waislamu wa Marekani wana hatari ya kunyanyaswa zaidi mwezi wa Ramadhani
May 10, 2018 14:31Baraza la Uhusiano wa Marekani na Uislamu limetaka kuchukuliwa hatua za lazima za kuimarisha usalama kwa ajili ya kuwalinda Waislamu ambao wana hatari ya kukumbwa na mashambulizi na unyanyasaji zaidi katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
Upinzani Uganda waijia juu serikali kwa mauaji ya viongozi wa Kiislamu
May 04, 2018 07:24Viongozi wa upinzani nchini Uganda wameitaka serikali ya Kampala kutoa ripoti kuhusu mauaji na kamatakamata dhidi ya viongozi na wahubiri wa Kiislamu katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki.
-
Viongozi wa Kiislamu Ufaransa wakosoa wito wa 'kufutwa' baadhi ya aya za Qurani
Apr 28, 2018 07:56Viongozi wa Kiislamu nchini Ufaransa wamekosoa vikali ombi lililowasilishwa na shakhsia 300 wa Ufaransa waliotaka kuondolewa baadhi ya aya katika kitabu kitakatifu cha Qur'ani kwa madai kuwa ni za kichochezi na zilizopitwa na wakati.
-
Siasa za Trump zaendelea kuchochea ukati dhidi ya Waislamu Marekani
Apr 25, 2018 02:32Uchunguzi uliofanyika hivi karibuni umeonesha kuwa, kuongezeka kwa ukatili na jinai zinazotokana na chuki dhidi ya Waislamu nchini Marekani kuna mfungamano na siasa za Rais wa sasa wa nchi hiyo, Donald Trump.
-
Waislamu Ufaransa walaani makala iliyopotosha Qur'ani tukufu
Apr 24, 2018 16:29Waislamu nchini Ufaransa wamelaani vikali kitendo cha kuchapishwa makala iliyovunjia heshima na kupotosha kitabu kitakatifu cha Qur'ani nchini humo.
-
Ripoti: Ofisi ya John Bolton imehusika kueneza habari za uongo dhidi ya Waislamu
Apr 24, 2018 07:30Televisheni moja ya nchini Marekani imetangaza kwamba, ofisi ya John R. Bolton, Mshauri wa Usalama wa Taifa wa ikulu ya Marekani White House, ndiyo inayohusika kueneza habari zisizo na ukweli dhidi ya Waislamu duniani.