-
Ndugu watatu Waislamu wateremshwa kwenye ndege kwa kutuhumiwa kuwa wanachama wa Daesh
Aug 24, 2016 10:29Ndugu watatu Waislamu raia wa Uingereza wamefikwa na mkasa wa kuteremshwa kwenye ndege katika uwanja wa ndege wa London na kuhojiwa kwa muda wa saa nzima baada ya abiria wenzao kuwatuhumu kuwa ni wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh.
-
Waziri Mkuu wa Ufaransa aunga mkono marufuku ya 'burqini'
Aug 17, 2016 23:09Waziri Mkuu wa Ufaransa ameunga mkono hatua ya mameya wa miji minne nchini humo kupiga marufuku vazi la stara la kuogelea linalovaliwa na wanawake wa Kiislamu linalofahamika kama 'burqini'.
-
Utafiti: Uislamu ndiyo dini inayokuwa kwa kasi zaidi duniani
Aug 17, 2016 09:36Utafiti uliofanywa na kituo cha utafiti cha Pew Research Center cha Marekani umeonyesha kuwa, Uislamu utasalia kuwa dini yenye kukuwa kwa kasi zaidi duniani katika kipindi cha miongo kadhaa ijayo.
-
Imam na msaidizi wake wauawa kwa risasi New York, Marekani
Aug 14, 2016 02:35Imam wa msikiti mmoja katika jimbo la New York nchini Marekani ameuawa kwa kufyatuliwa risasi katika mazingira ya kutatanisha.
-
Askari waliostaafu Marekani watishia kuwachinja Waislamu Texas
Aug 09, 2016 09:17Wanajeshi waliostaafu katika jimbo la Texas nchini Marekani wametishia kuwakata vichwa kwa mapanga Waislamu watakaoenda kutekeleza ibada ya swala katika msikiti mmoja jimboni hapo.
-
Waislamu nchini Nigeria waandamana kutaka Sheikh Ibrahim Zakzaky aachiliwe huru
Aug 08, 2016 10:12Waislamu nchini Nigeria wameendelea kufanya maandamano ya amani wakitaka kuachiliwa huru Sheikh Ibrahim Zakzaky, Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya nchi hiyo aliyewekwa kizuizini na vikosi vya usalama vya nchi hiyo.
-
Ripoti: Askari walioua Waislamu Nigeria washtakiwe
Aug 02, 2016 03:00Jopo la uchunguzi lililotwika jukumu la kuchunguza mauaji ya Waislamu kaskazini mwa Nigeria limekiri kuwa jeshi la nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika liliuawa Waislamu zaidi ya 300 katika mji wa Zaria jimbo la Kaduna.
-
Waislamu wa Marekani; kitovu cha kinyang'anyiro cha uchaguzi wa rais
Aug 01, 2016 02:20Hotuba ya Khizr Khan, baba wa askari mmoja Mmarekani Muislamu aliyeuawa katika vita vya Iraq, kwa mara nyengine tena imeifanya hali na nafasi ya Waislamu kuwa kitovu cha kinyang'anyiro cha uchaguzi wa rais wa nchi hiyo.
-
Bahrain yaendeleza ubabe, yamkamata kiongozi mwingine wa Kiislamu
Jul 30, 2016 03:40Licha ya makelele ya jamii ya kimataifa na watetezi wa haki za binadamu, utawala wa Aal-Khalifa nchini Bahrain umemtia nguvuni kiongozi mwingine wa Kiislamu.
-
Waislamu Nigeria wapongeza kuondolewa marufuku ya hijabu
Jul 24, 2016 03:30Waislamu nchini Nigeria wamepongeza uamuzi wa Mahakama ya Rufaa mjini Lagos kufutulia mbali marufuku ya kuvaa hijabu katika shule za umma mjini hapo.