-
Zarif: Masunni na Mashia lazima waungane kuzima ugaidi
Jul 24, 2016 00:00Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani hujuma ya kigaidi ya hapo jana iliyosababisha vifo vya makumi ya watu nchini Afghanistan na kusisitiza kuwa, wakati umefika kwa Waislamu wa madhehebu ya Shia na Sunni waungane kwa shabaha ya kulikabili kwa pamoja jinamizi la ugaidi.
-
Bahrain yazuia Swala ya Ijumaa na kukamata watu 50 Diraz
Jul 22, 2016 23:37Katika muendelezo wa wimbi la ukandamizaji na dhulma za utawala wa kifalme wa Aal-Khalifa, maafisa usalama nchini Bahrain walizuia Swala ya Ijumaa hapo jana sambamba na kuwatia mbaroni watu 50 katika kijiji cha Diraz, kaskazini magharibi mwa nchi.
-
Waziri Mkuu wa Ufaransa aonya kuhusu hujuma dhidi ya Waislamu nchini humo
Jul 21, 2016 23:49Waziri Mkuu wa Ufaransa ameonya kuhusu hatari ya kuhujumiwa Waislamu wanaoishi nchini humo.
-
Msomi wa Kisunni Iran atoa wito wa kuugwa mkono Waislamu Kashmir
Jul 21, 2016 23:47Msomi wa Kisunni ambaye pia ni mwanachama wa Baraza la Wataalamu la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa wito kwa Waislamu kote duniani kulaani mauaji ya hivi karibuni ya ndugu zao wa eneo la Kashmir linalodhibitiwa na India.
-
Waziri Mkuu Ufaransa: Kuna hatari Waislamu wakashambuliwa
Jul 21, 2016 02:14Waziri Mkuu wa Ufaransa ametahadharisha kuhusu hatari ya kushambuliwa Waislamu nchini humo.
-
Waislamu Marekani waanzisha kampeni dhidi ya Trump
Jul 21, 2016 01:51Waislamu wa Marekani wameanzisha "Harakati ya Kura Milioni Moja" kwa shabaha ya kukabiliana na misimamo inayopiga vita Uislamu ya mgombea urais wa nchi hiyo kwa tiketi ya chama cha Republican, Donald Trump.
-
Rais Sally: Waislamu ni wahanga wakubwa wa ugaidi
Jul 17, 2016 03:36Rais wa Senegal amesema kuwa Waislamu ni wahanga wakubwa wa ugaidi duniani.
-
Newt Gingrich: Waislamu wafukuzwe Marekani
Jul 16, 2016 00:06Spika wa zamani wa Kongresi ya Marekani amesema kuwa Waislamu wanaoshikamana na sheria za Kiislamu wanapaswa kufukuzwa nchini Marekani.
-
Waislamu Uingereza washtushwa na kuteuliwa Bi. May kama Waziri Mkuu
Jul 14, 2016 02:00Waislamu nchini Uingereza wameshtushwa na kuteuliwa Bi. Theresa May kama Waziri Mkuu kutokana na sera zake haribifu kwa jamii ya Waislamu nchini humo.
-
Viogozi wa Waislamu Kenya walalamikia safari ya Netanyahu
Jul 10, 2016 02:17Viongozi wa Waislamu nchini Kenya wamekosoa vikali uhusiano wa nchi yao na utawala wa Kizayuni wa Israel pamoja na ziara ya hivi karibuni ya Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala huo dhalimu katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki.