Viktor Orbán, Waziri Mkuu wa Hungary amesema katika taarifa kwamba viongozi wa Umoja wa Ulaya na Jumuiya ya Kujihami ya Kijeshi ya Magharibi (NATO) wanauchukulia mzozo wa Moscow na Kyiv kuwa ni wao na wala hawazingatii hatari ya kujihusisha na mzozo huo. Ameonya kuwa NATO inakaribia kutuma askari wake huko Ukraine.
Ireland ilitangaza Jumatano, Machi 27, kwamba itashiriki katika kesi iliyowasilishwa na Afrika Kusini katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) dhidi ya utawala wa Isarel kutokana na mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na utawala huo huko Gaza.
Waziri Mkuu wa Serikali ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina Mohammad Ashtiyah, amejiuzulu wadhifa wake huo.
Pedro Sánchez, Waziri Mkuu wa Uhispania ameonya kuwa, usalama na uthabiti wa eneo la Asia Magharibi (Mashariki ya Kati) umekuwa hatarini na kwamba, mashambulizi haya yanahatarisha nidhamu na uratibu wa ushirikiano wa pande kadhaa.
Waziri Mkuu wa Iraq ameashiria hatua za kuvuruga usalama na amani vya Marekani na kutaka kuondoka nchini humo wanajeshi vamizi wa Marekani haraka iwezekanavyo.
Hatua ya Uhispania na Ubelgiji ya kutangaza kuwa tayari kuitambua rasmi nchi huru ya Palestina ni tukio muhimu kushuhudiwa barani Ulaya kuhusu kadhia ya Palestina. Hatua hii imeukasirisha sana utawala wa Kizayuni.
Waziri Mkuu wa Ireland, Leo Varadkar amekosoa vikali undumilakuwili wa nchi za Magharibi na kusema kuwa Umoja wa Ulaya na madola ya Magharibi yanashughulikia masuala yanayohusiana na Israel na Palestina kwa undumilakuwili wa wazi.
Waziri Mkuu wa Iraq amesisitiza kwa mara nyingine tena kwamba nchi yake haitageuzwa kuwa sehemu ya kukika mamlaka ya kujitawala ya nchi yoyote ile hasa nchi jirani.
Waziri Mkuu wa Kuwait Ahmad Nawaf Al-Ahmad Al-Sabah amesisitiza kuwa Palestina ni moja ya masuala muhimu katika ulimwengu wa Kiislamu na ulimwengu wa Kiarabu.
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran ametilia mkazo kuanzishwa utaratibu wa kutumia sarafu ya Riyali na Rupia katika mabadilishano ya kibiashara na kiuchumi kati ya Iran na India.