Oct 24, 2022 04:00
Giorgia Meloni amepewa rasmi jukumu la uwaziri mkuu wa Italia kutoka chama chenye misimamo mikali ya kulia cha Brothers of Italy. Hayo yamekuja baada ya kufanyika mazungumzo ya pande kadhaa na hatimaye Rais wa Italia amempa jukumu Meloni la kuunda serikali mpya akiwa ni Waziri Mkuu wa kwanza kabisa mwanamke katika historia ya Italia.