-
Mzimbabwe adai kutibu UKIMWI, WHO yasisitiza hakuna tiba
Nov 01, 2018 06:52Shirika la Afya Duniani WHO limesema hadi sasa hakuna tiba ya ugonjwa hatari wa Ukimwi na wagonjwa nchini Zimbabwe wanaotumia dawa za kupunguza makali ya virusi vinavyosababisha ugonjwa huo, VVU waendelee kuzitumia.
-
Upizani Zimbabwe: Rais Mnangagwa hana uhalali wa kuongoza
Oct 24, 2018 02:52Kiongozi wa chama cha upinzani cha MDC nchini Zimbabwe, Nelson Chamisa ametoa mwito wa kuundwa Mamlaka ya Kitaifa ya Mpito akisisitiza kuwa hiyo ndiyo njia pekee ya kuupatia ufumbuzi mgogoro kuhusu uhalali wa serikali ya Rais Emmerson Mnangagwa.
-
Mnangagwa: Kodi mpya inahitajika kwa ajili ya kufufua uchumi
Oct 09, 2018 02:34Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe amesema kuwa kodi mpya kwa malipo ya kielektroniki iliyotangazwa nchini humo inaumiza lakini ni sehemu muhimu ya jitihada za serikali za kufufua uchumi.
-
China: Hatuna azma ya 'kuikoloni' Zimbabwe licha ya kushindwa kutulipa madeni yetu
Oct 02, 2018 08:19China imesema Beijing haina nia wala mpango wa kunyakua na kudhibiti mali za Zimbabwe licha ya serikali ya Harare kushindwa kuilipa nchi hiyo malimbikizo ya madeni yake.
-
WHO: Idadi ya walioaga dunia kwa kipindupindu Zimbabwe yafikia 45
Sep 26, 2018 08:01Watu wasiopungua 45 wamepoteza maisha kwa ugonjwa wa kipindupindu nchini Zimbabwe wiki tatu zilizopita. Hayo yameelezwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) huku likitaja aina hiyo ya mlipuko wa waba kuwa wenye kushindikana kutibika kwa aina mbalimbali za dawa.
-
Wabunge wa upinzani Zimbabwe wasusia hotuba ya Rais Mnangagwa
Sep 18, 2018 14:42Wabunge wa kambi ya upinzani nchini Zimbabwe mapema leo wameondoka bungeni na kususia hotuba ya Rais wa nchi hiyo, Emmerson Mnangagwa, ikiwa ni ishara ya hasira zao dhidi ya matokeo ya uchaguzi uliozusha utata wa rais ambayo yalimpa ushindi kiongozi wa chama tawala.
-
Kiongozi wa upinzani Zimbabwe aakhirisha kula kiapo
Sep 14, 2018 23:58Kiongozi mkuu wa upinzani nchini Zimbabwe ameakhirisha mipango ya kushiriki katika hafla ya kujiapisha kama rais wa nchi iliyokuwa imepangwa kufanyika leo (Jumamosi) baada ya polisi kupiga marufuku mikutano na mijumuiko ya wananchi kufuatia nchi hiyo kuathiriwa na mlipuko wa kipindupindu kilichouwa watu 26 hadi sasa.
-
Marekani: Vikwazo dhidi ya Zimbabwe vitaendelea kuwepo
Sep 14, 2018 15:45Serikali ya Marekani haitaondoa vikwazo ilivyoiwekea Zimbabwe hadi pale serikali mpya ya Rais Emmerson Mnangagwa wa nchi hiyo itakapodhihirisha kuwa inabadili mielekeo yake. Hayo yameelezwa na afisa wa ngazi ya juu wa masuala ya uchumi wa Marekani.
-
Polisi ya Zimbabwe yapiga marufuku mikusanyiko mjini Harare baada ya kuenea kipindupindu
Sep 13, 2018 07:41Polisi ya Zimbabwe imepiga marufuku mikusanyiko ya aina yoyote ile katika mji mkuuu Harare baada ya kipindipindu kusambaa mjini humo na kuua watu wasiopungua 21 hadi sasa.
-
Zimbabwe yatangaza hali ya hatari baada ya kuzuka kipindupindu katika mji mkuu Harare
Sep 12, 2018 03:53Serikali ya Zimbabwe imetangaza hali ya hatari baada ya kuibuka maradhi ya kipindupindu katika mji mkuuu Harare.