Hizbullah ya Lebanon yathibitisha kuuawa shahidi Sayyid Hashim Safiyyuddin
(last modified Thu, 24 Oct 2024 02:14:25 GMT )
Oct 24, 2024 02:14 UTC
  • Sayyid Hashem Safiyyuddin
    Sayyid Hashem Safiyyuddin

Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon imetoa taarifa na kuthibitisha kuuawa shahidi Mkuu wake wa Baraza la Utendaji katika shambulio lililofanywa na utawala wa Kizayuni kwenye kitongoji Adh-Dhaahiyah Kusini katika mji mkuu wa nchi hiyo Beirut.

Kwa mujibu wa ripoti ya Mtandao wa Sahab iliyonukuu shirika la habari la IRNA, Hizbullah ya Lebanon imeeleza katika taarifa kwamba: "Sayyid Hashem Safiyyuddin", Mkuu wa Baraza la Utendaji la harakati hii ameuawa shahidi katika shambulio la utawala wa Kizayuni dhidi ya Beirut".
 
Taarifa ya Hizbullah imeendelea kusema: "tunatoa pole kwa taifa la mashahidi na mujahidina, taifa la Muqawama na ushindi, kwa kuuawa shahidi kiongozi mkubwa na shahidi mkubwa wa njia ya Quds, Mkuu wa Baraza la Utendaji la Hizbullah, Sheikh Seyyed Hashim Safiyyuddin. 

Taarifa hiyo ya Hizbullah imeendelea kueleza: Sayyid Hashem Safiyyuddin alitumia muda mwingi zaidi wa maisha yake katika njia ya kuitumikia Hizbullah na Muqawama wa Kiislamu na jamii yake; na katika kipindi cha miaka mingi ya uhai wake mtukufu, kwa uwajibikaji na uwezo kamili, aliliongoza Baraza la Utendaji, taasisi na vitengo vyake.

Kwa kumalizia taarifa yake hiyo, mbali na Hizbullah kuthibitisha tena mkono wa ahadi na baia' iliotoa kwa shahidi huyo mtukufu, imesisitiza kwamba itaendeleza njia ya Muqawama na Jihadi hadi malengo yake yatakapofikiwa ya ukombozi na ushindi.../

Tags