Mwandishi aliposhambuliwa kwa kombora akiwa hewani mubashara
https://parstoday.ir/sw/news/west_asia-i26624-mwandishi_aliposhambuliwa_kwa_kombora_akiwa_hewani_mubashara
Mwandishi wa televisheni ya al Alam, Haydar Qassim amejeruhiwa mguuni baada ya eneo alipokuwa anatoa ripoti yake kwa sura ya mubashara kushambuliwa kwa kombora na magaidi wa Daesh, magharibi mwa Mosul, kaskazini mwa Iraq.
(last modified 2026-02-21T22:51:18+00:00 )
Mar 20, 2017 07:53 UTC

Mwandishi wa televisheni ya al Alam, Haydar Qassim amejeruhiwa mguuni baada ya eneo alipokuwa anatoa ripoti yake kwa sura ya mubashara kushambuliwa kwa kombora na magaidi wa Daesh, magharibi mwa Mosul, kaskazini mwa Iraq.

Mkanda huu wa video unamuonesha mwandishi Haydar na timu yake wakishuhudia kwa karibu mashambulizi kadhaa ya makombora ya magaidi wa ISIS wakati wakiwa hewani. Hata hivyo wameendelea kuripoti katika eneo lililo karibu zaidi na mapigano magharibi mwa Mosul, licha ya kukumbwa na mashambulizi hayo.