Familia za Daesh zakimbia kaskazini mwa mkoa wa Salahuddin Iraq
https://parstoday.ir/sw/news/west_asia-i33909-familia_za_daesh_zakimbia_kaskazini_mwa_mkoa_wa_salahuddin_iraq
Sambamba na kukaribia wakati wa kutekelezwa oparesheni ya kuukomboa mji wa Shirqat katika mkoa wa Salahhudin huko kaskazini mwa Iraq, familia za magaidi wa kundi la Daesh zimeripotiwa kulikimbia eneo hilo usiku kucha.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Sep 03, 2017 23:13 UTC
  • Familia za Daesh zakimbia  kaskazini mwa mkoa wa  Salahuddin Iraq

Sambamba na kukaribia wakati wa kutekelezwa oparesheni ya kuukomboa mji wa Shirqat katika mkoa wa Salahhudin huko kaskazini mwa Iraq, familia za magaidi wa kundi la Daesh zimeripotiwa kulikimbia eneo hilo usiku kucha.

Ripoti zinasema kuwa kukombolewa kikamilifu mji wa Tal Afar kumetoa pigo kubwa kwa makamanda na wanachama wa Daesh na kuwalazimisha kukimbia.  Ukanda wa kushoto wa mji wa Shirqat unadhibitiwa na magaidi wa Daesh tangu mwezi Julai mwaka 2014 hadi sasa, na  sasa jeshi la Iraq linajiandaa kuukomboa kutoka mikononi mwa magaidi hao.

Wanajeshi wa Iraq katika oparesheni ya kuukomboa mji wa Tal Afar 

Haidar al Abadi Waziri Mkuu wa Iraq na ambaye pia ni Amiri Jeshi wa majeshi ya nchi hiyo siku kadhaa zilizopita alitangaza rasmi kupatikana ushindi wa mwisho dhidi ya Daesh huko Tal Afar.