Familia za Daesh zakimbia kaskazini mwa mkoa wa Salahuddin Iraq
Sambamba na kukaribia wakati wa kutekelezwa oparesheni ya kuukomboa mji wa Shirqat katika mkoa wa Salahhudin huko kaskazini mwa Iraq, familia za magaidi wa kundi la Daesh zimeripotiwa kulikimbia eneo hilo usiku kucha.
Ripoti zinasema kuwa kukombolewa kikamilifu mji wa Tal Afar kumetoa pigo kubwa kwa makamanda na wanachama wa Daesh na kuwalazimisha kukimbia. Ukanda wa kushoto wa mji wa Shirqat unadhibitiwa na magaidi wa Daesh tangu mwezi Julai mwaka 2014 hadi sasa, na sasa jeshi la Iraq linajiandaa kuukomboa kutoka mikononi mwa magaidi hao.
Haidar al Abadi Waziri Mkuu wa Iraq na ambaye pia ni Amiri Jeshi wa majeshi ya nchi hiyo siku kadhaa zilizopita alitangaza rasmi kupatikana ushindi wa mwisho dhidi ya Daesh huko Tal Afar.