-
Waziri Mkuu wa Iraq akosoa mauaji Ghaza na Lebanon na vitisho dhidi ya Iran
Jan 18, 2026 07:03Waziri Mkuu wa Iraq amekosoa vikali unyama na mauaji ya kigaidi huko Ghaza na Lebanon, mashambulizi yanayoendelea kufanywa na Israel nchini Syria, pamoja na tishio dhidi ya Iran ambayo ni nchi jirani na Iraq.
-
Amr Moussa atoa indhari kali kwa Saudia na Misri kuhusiana na utawala wa kizayuni wa Israel
Jan 18, 2026 03:11Katibu Mkuu wa zamani wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu ametoa indhari kali kwa Saudi Arabia na Misri kuhusiana na hatua zinazochukuliwa na utawala wa kizayuni wa Israel na akasema: kinachojiri hivi sasa si suala dogo na la pembeni bali ni "tishio la kimkakati" kwa usalama wa nchi za Kiarabu na eneo kwa ujumla.
-
Marekani yatangaza wajumbe wa iitwayo 'Bodi ya Amani' ya Ghaza, yumo pia Tony Blair
Jan 18, 2026 02:39Ikulu ya White House imetangaza majina ya wajumbe wa linaloitwa baraza la amani litakaloongozwa na Rais wa Marekani Donald Trump na kusimamia utawala wa eneo la Palestina la Ukanda wa Ghaza. Orodha hiyo inajumuisha waziri wa mambo ya nje wa Marekani Mark Rubio, mjumbe maalumu wa Trump Steve Witkoff, mkwe wa Trump Jared Kushner, na waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Tony Blair.
-
Mchambuzi Mzayuni: Marekani haina uthubutu wa kuanzisha vita vingine dhidi ya Iran
Jan 17, 2026 02:31Mchambuzi mmoja wa masuala ya kieneo na kimataifa wa utawala wa Kizayuni amesema kuwa, si Donald Trump na si Marekani yenyewe, wote hawana uthubutu wa kuanzisha vita vipya dhidi ya Iran.
-
Jumuiya ya Shanghai yalaani ghasia za kigaidi nchini Iran huku uungaji mkono kimataifa ukiongezeka
Jan 16, 2026 07:18Norlan Yerkembayev Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai (SCO) amelaani vikali hujuma za kigaidi na uharibifu wa hivi karibuni katika mji wa Tehran na miji mingine ya Iran iliyoathiriwa wakati wa maandamano ya amani ya wananchi.
-
Kiongozi wa Ansarullah: Taifa la Iran limetibua njama ya adui kwa maandamano ya mamilioni ya wananchi
Jan 16, 2026 07:15Kiongozi wa harakati ya muqawama ya Ansarullah ya Yemen amesema kuwa Marekani na Israel ziliwaweka magaidi vibaraka wao ili kuchochea machafuko Iran kupitia kuchoma moto misikiti na kuuwa vikosi vya usalama na raia hata hivyo taifa la Iran limetoa jibu madhubuti kwa hujuma hiyo kwa maandamano makubwa ya mamilioni ya wananchi kote nchini kulaani ghasia na machafuko.
-
Kamati ya Wateknokrati wa kuendesha Ghaza kukutana kwa kikao cha kwanza mjini Cairo, Misri
Jan 15, 2026 10:28Mipango inaendelea kupangwa kuhakikisha wajumbe wa kamati ya wateknokrati iliyoteuliwa kuendesha masuala ya Ghaza kusafiri hadi Misri kwa mkutano wake wa kwanza, uliotarajiwa kufanyika leo Alkhamisi au kesho Ijumaa. Hayo ni kwa mujibu wa chanzo kimoja cha habari cha Palestina.
-
Shirika la UNICEF: Watoto wa Gaza wamesahauliwa na jamii na kimataifa
Jan 14, 2026 11:47Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) umetangaza kuwa, jamii ya imewasahau watoto wa Gaza ambao wanataabika na kuteteseka kutokana na kukabiliwa na hali mbaya ya kibinadamu na ukatili wa kutisha.
-
Qatar: Tunawasiliana ili kutatua tofauti kati ya Marekani na Iran
Jan 14, 2026 02:42Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar ametangaza kuwa, Doha inafanya mawasiliano na pande mbalimbali ili kutuliza hali katika eneo hili na kutatua tofauti kati ya Iran na Marekani.
-
Wanasiasa wa Pakistan: Ulimwengu wa Kiislamu unapaswa kusimama pamoja na Iran
Jan 14, 2026 02:41Wanasiasa mbalimbali wa Pakistan wamesisitiza kuwa, ulimwengu wa Kiislamu unapaswa kuwa upande wa Iran katika mazingira ya sasa ambapo taifa hili la Kiislamu linaandamwa kwa njama mbalimbali.