-
Sheikh Qassem: Hizbullah haina lengo la kuanzisha vita, lakini kamwe haitasalimu amri
Feb 17, 2026 07:07Sheikh Naim Qassim Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa harakati hiyo ya muqawama haitaki vita lakini imejiandaa kikamilifu kuilinda Lebanon na kutoa jibu kali kwa uchokozi wowote wa maadui wa nchi hiyo.
-
Mijibizo dhidi ya njama za Israel za kuendeleza uporaji na ukaliaji wa mabavu wa ardhi za Ukingo wa Magharibi
Feb 17, 2026 02:24Makundi ya Wapalestina na nchi kadhaa za eneo zimetoa mjibizo kwa mpango wa utawala wa Kizayuni wa Israel wa kuvamia na kuyakalia kwa mabavu maeneo kadhaa ya ardhi za Ukingo wa Magharibi, zikisisitiza kwamba, huo ni ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa.
-
"Ni muhali kufikia amani na Israel madhali inakiuka haki za Wapalestina"
Feb 16, 2026 10:17Waziri wa Mambo ya Nje na Wahamiaji wa Palestina, Varsen Aghabekian Shahin amesema kufikia amani na Israel "haiyumkiniki" madhali haki za Wapalestina zinakiukwa na utawala huo wa Kizayuni, akisisitiza kwamba sheria za kimataifa zinapasa kuzingatiwa, na uchukuaji wa hatua za upande mmoja lazima ukomeshwe.
-
Palestina yapongeza matokeo ya mkutano wa kilele wa Afrika uliounga mkono uanachama wake UN
Feb 16, 2026 05:58Palestina imekaribisha matokeo ya mkutano wa kilele wa Umoja wa Afrika uliofanyika Addis Ababa, ambao umesisitiza tena upinzani wa bara hilo dhidi ya mipango ya kuwafukuza Wapalestina katika nchi yao na kuunga mkono suala la Palestina kupata uanachama kamili katika Umoja wa Mataifa.
-
Msemaji wa serikali ya Afghanistan: Tutaiunga mkono Iran kama itakabiliwa na uadui
Feb 16, 2026 05:55Msemaji wa serikali ya Afghanistan amesisitiza kwamba watu wa Afghanistan wataonyesha mshikamano na kutoa aina mbalimbali za misaada kwa Iran iwapo kutatokea uchokozi wowote dhidi ya nchi hiyo.
-
Palestina yataka uingiliaji kati wa walimwengu kusitisha mashambulizi ya Israel
Feb 16, 2026 03:31Mamlaka ya Ndani ya Palestina, imetoa radiamali kwa uamuzi wa baraza la mawaziri la utawala wa Kizayuni wa Israel kuhusu kutaifisha ardhi za Ukingo wa Magharibi na kuitaka jamii ya kimataifa kuchukua hatua kuhusu suala hilo.
-
Wapalestina 10 wauawa katika mashambulizi ya Israel Gaza licha ya usitishaji vita
Feb 16, 2026 02:57Vikosi vya Israel vimewaua angalau Wapalestina 10 katika mashambulizi mapya yaliyofanywa katika maeneo mbalimbali ya Ukanda wa Gaza, katika ukiukaji mwingine wa makubaliano ya usitishaji vita yaliyoratibiwa na Marekani na kuanza kutekelezwa Oktoba 10 mwaka jana.
-
Mvutano waongezeka kati ya Netanyahu na Herzog baada ya Trump kumtusi Rais wa Israel
Feb 15, 2026 11:33Hatua ya Rais Donald Trump wa Marekani ya kumtusi Rais wa utawala wa kizayuni wa Israel akimuunga mkono waziri mkuu wa utawala huo yameongeza mvutano kati ya Netanyahu na Isaac Herzog.
-
Katibu Mkuu wa Hizbollah: Iran daima imekuwa ikiunga mkono Palestina na wanyonge duniani
Feb 15, 2026 10:59Katibu Mkuu wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Hizbollah ya Lebanon amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imekuwa ikiunga mkono Palestina na watu wanaokandamizwa duniani.
-
"Hatuui tu, tunabaka": Mwanajeshi wa Israel aliyeua watu Gaza akiri kufanya uhalifu
Feb 15, 2026 10:24Mwanajeshi mmoja katika jeshi la Israel ametoa kauli ya kushtua katika mahojiaano ya moja kwa moja na YouTuber wa Marekani, akizungumzia vitendo vinavyofanywa na wanajeshi wa utawala huo dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza katika vita vya mauaji ya kimbari.