-
Mradi wa reli ya Ankara–Riyadh waibua wasiwasi Israel
Jun 14, 2026 03:02Pendekezo la kuanzisha ukanda mpya wa biashara na usafirishaji unaoendelezwa na Uturuki na Saudi Arabia limeibua wasiwasi miongoni mwa maafisa wa utawala wa Israel.
-
Amnesty International: Israel inafanya "maangamizi ya kizazi" katika Ukingo wa Magharibi
Jun 13, 2026 09:04Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limekutaja kuongezeka vitendo vya ukatili vya utawala wa Israel dhidi ya Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi kuwa ni "maangamizi ya kizazi" na "kulazimisha watu kuhama makazi yao."
-
Hizbullah: Tuna imani Iran itailinda Lebanon katika makubaliano yoyote na Marekani
Jun 13, 2026 02:42Makubaliano yoyote kati ya Iran na Marekani yatakuwa na matokeo ya moja kwa moja kwa Lebanon bila kujali kuwa mamlaka za Lebanon zinakubali au la.
-
Kwa nini watawala wa Marekani wanajaribu kujitenga na chokochoko za Netanyahu?
Jun 10, 2026 12:22Kushirikiana kwa utawala wa Trump na vitendo vya jinai na uchokozi vya Israel katika kipindi cha miaka miwili iliyopita kumekuwa na taathira mbaya kwa msimamo wa serikali ya sasa ya Marekani mbele ya maoni ya umma ndani na nje ya nchi hiyo.
-
Italia yaanzisha uchunguzi dhidi ya Ben-Gvir kuhusu unyanyasaji wa wanaharakati wa Global Sumud Flotilla
Jun 10, 2026 03:59Waendesha mashtaka wa Italia wameanzisha uchunguzi dhidi ya Waziri wa Usalama wa Israel mwenye msimamo mkali wa mrengo wa kulia, Itamar Ben-Gvir kuhusu mateso, unyanyasaji na utekaji nyara wa wanaharakati walioshiriki katika msafara wa Global Sumud Flotilla wa kupeleka misaada ya kibinadamu kwa watu wa Gaza, mwezi uliopita.
-
Hamas yaonya kuhusu ongezeko la ubomoaji wa majengo Ukingo wa Magharibi, yataka hatua za kimataifa zichukuliwe dhidi ya Israel
Jun 10, 2026 03:55Harakati ya Hamas imeonya kuhusu ongezeko la shughuli za ubomoaji wa nyumba na majengo ya Wapalestina unaofanywa na Israel katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu, ikiwa ni pamoja na al-Khalil, ikitaja vitendo hivyo kuwa ni ukiukaji wa sheria za kimataifa.
-
Spika wa Bunge la Lebanon ataka kuondoka Israel nchini humo huku Hizbullah ikifichua madai ya uwongo ya Trump
Jun 10, 2026 03:43Spika wa Bunge la Lebanon amesema kuwa nchi hiyo haitakubali chochote isipokuwa usitishaji vita kamili na usio na masharti kwa upande wa ardhini, anga na baharini, na kusisitiza msimamo thabiti wa Muqawama wa Lebanon dhidi ya hujuma za Israel.
-
Yemen yatangaza marufuku ya meli za Israel katika Bahari ya Sham
Jun 08, 2026 11:13Vikosi vya Jeshi la Yemen vimetangaza marufuku kamili ya usafiri wa baharini wa Israel katika Bahari Nyekundu (Bahari ya Sham), vikisema kwamba harakati zote za adui katika eneo hilo sasa zitachukuliwa kuwa malengo halali ya kijeshi, baada ya kutekeleza shambulizi la kombora lenye usahihi dhidi ya maeneo nyeti ya Israel huko Tel Aviv.
-
Waandishi wa habari wa Gaza wasimulia unyanyasaji waliokumbana nao katika gereza la Israel
Jun 07, 2026 03:50Shirika la Waandishi wa Habari Wasio na Mipaka (RSF) limechapisha ushuhuda kutoka kwa waandishi wa habari watano wa Kipalestina huko Gaza, ambao walitekwa nyara na askari wa Israel baada ya Oktoba 7, 2023 ikiwa ni pamoja na visa vya unyanyasaji, kuhojiwa na ukiukwaji wa sheria unaohusiana moja kwa moja na shughuli zao za uandishi wa habari.
-
Israel na walowezi wa Kizayuni wazidisha mashambulizi katika Ukingo wa Magharibi
Jun 07, 2026 03:18Wanajeshi wa Israel na walowezi wa Kizayuni wamezidisha mashambulizi yao dhidi ya Wapalestina katika eneo la Ukingo wa Magharibi linalokaliwa kwa mabavu.