-
"Hatuui tu, tunabaka": Mwanajeshi wa Israel aliyeua watu Gaza akiri kufanya uhalifu
Feb 15, 2026 10:24Mwanajeshi mmoja katika jeshi la Israel ametoa kauli ya kushtua katika mahojiaano ya moja kwa moja na YouTuber wa Marekani, akizungumzia vitendo vinavyofanywa na wanajeshi wa utawala huo dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza katika vita vya mauaji ya kimbari.
-
Israel yakasirishwa na kauli ya kumdhalilisha rais wake iliyotolewa na Trump
Feb 15, 2026 03:26Duru zilizo karibu na rais wa utawala wa kizayuni wa Israel zimeyaelezea matamshi ya Rais wa Marekani Donald Trump ya kumtusi na kumdhalilisha rais wa utawala huo Isaac Herzog kuwa ni uvukaji mistari myekundu.
-
Ripota maalumu wa UN: Hujuma dhidi yangu si chochote kulinganisha na mateso ya Wapalestina
Feb 14, 2026 09:56Francesca Albanese, Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya haki za binadamu katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu amesema, analengwa na hujuma za kumchafulia jina na kumtaja kwa ubaya kwa sababu ya kulaani vita vya utawala wa kizayuni wa Israel dhidi ya Ghaza na Ukingo wa Magharibi.
-
Ulinzi wa Raia Gaza: Miili 8,000 ya mashahidi wa mauaji ya kimbari bado imefunikwa na vifusi
Feb 14, 2026 06:21Idara ya Ulinzi wa Raia katika Ukanda wa Gaza inasema kuwa maelfu ya miili ya Wapalestina waliouawa katika mashambulizi ya Israel bado imezikwa chini ya magofu ya majengo yaliyoharibiwa katika eneo hilo la Palestina, huku timu za uokoaji zikijitahidi kufika kwenye vitongoji vilivyoharibiwa wakati wa vita vya mauaji ya kimbari vya utawala wa Israel.
-
Al Houthi: Iran ni ngome imara inayokwamisha njama za Marekani na Israel
Feb 14, 2026 04:14Kiongozi wa harakati ya Kiislamu ya Ansarullah nchini Yemen amesema kuwa Marekani na Utawala wa Israel zinakabiliana na Iran kwa sababu Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inasimama kama kizuizi dhidi ya mradi wao mpana wa kutawala eneo la Asia Magharibi.
-
Chama cha Jamaat-e-Islami nchini Bangladesh chatilia shaka matokeo ya uchaguzi
Feb 14, 2026 02:23Chama cha Jamaat-e-Islami, chama kikubwa zaidi cha Kiislamu nchini Bangladesh, kimehoji matokeo ya uchaguzi uliofanyika nchini humo majuzi, ambapo kimeshika nafasi ya pili kwa kupata viti 74 baada ya Chama cha Kizalendo cha Bangladesh, ambacho kumeshinda viti 212 kati ya 300 vya Bunge.
-
Iran yalaani juhudi za Israel za kunyakua Ukingo wa Magharibi, yasema ni 'maangamizi ya kizazi ya kikoloni'
Feb 14, 2026 02:23Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani vikali uamuzi wa hivi karibuni wa utawala ghasibu wa Israel wa kunyakua ardhi zaidi za Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu, ikisema hatua hiyo inalenga kupanua 'ujenzi wa vitongoji haramu' na kuimarish uvamizi na udhibiti wa masuala ya usalama katika eneo hilo, sambamba na kuendeleza 'mauaji ya kimbari' ya Gaza.
-
Palestina inavyotokomezwa kupitia ukoloni; Iran yalaani uamuzi wa Israel wa kunyakua Ukingo wa Magharibi
Feb 13, 2026 07:21Iran imelaani vikali uamuzi wa hivi karibuni wa utawala wa Israel wa kunyakua ardhi zaidi za Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu, ikisema kuwa hatua hiyo inalenga kupanua "ujenzi haramu wa vitongoji vya walowezi za Kizayuni" na kuimarisha ukaliaji mabavu na hatua kali za kiusalama dhidi ya Wapalestina na kuendelea "mauaji ya kimbari" huko Gaza.
-
Hamas yazionya US, Israel: Vita yoyote dhidi ya Iran ni sawa na kushambulia Ulimwengu mzima wa Kiislamu
Feb 12, 2026 11:23Brigedi za al Qassam, tawi ila kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imeonya kuwa vita yoyote dhidi ya Iran ni sawa na shambulio dhidi ya Umma mzima wa Kiislamu.
-
Wabangladesh washiriki katika uchaguzi wa kihistoria tangu kuangushwa utawala wa Hasina
Feb 12, 2026 06:30Upigaji kura unaendelea nchini Bangladesh katika uchaguzi unaoonekana kama mtihani muhimu wa kurejea kwa demokrasia nchini humo baada ya vuguvugu la umma lililoongozwa na wanafunzi kumng'oa madarakani kiongozi wa muda mrefu Sheikh Hasina mnamo Agosti 2024.