Rais wa Mexico amjibu Trump: Tuko tayari kwa ushirikiano, lakini hatukubali kamwe 'kutiishwa' na US
Rais wa Mexico Claudia Sheinbaum amekataa pendekezo la Rais wa Marekani Donald Trump la kupeleka wanajeshi ndani ya ardhi ya nchi hiyo kupambana na magenge ya madawa ya kulevya na akasisitiza kwamba, wakati Mexico imeweka mlango wazi kwa ushirikiano, haitakubali kamwe "kutiishwa" kwa Washington.
Akihutubia katika ufunguzi wa chuo kikuu Rais wa Mexico amethibitisha ripoti hiyo na kuweka wazi msimamo wake.
"Ni kweli" amesema Bi Sheinbaum, na akamnukuu Trump akisema: 'ninapendekeza jeshi la Marekani liingie kusaidia.' Na unajua nilichomwambia? "Hapana, Rais Trump, ardhi yetu haitolewi, mamlaka yetu ya kujitawala hayatolewi, mamlaka yetu ya kujitawala hayauzwi!"
Rais wa Mexico ameongeza kuwa, ikiwa Trump anataka kusaidia, ajikite katika kuzuia silaha zinazomiminika ndani ya Mexico zikitokea Marekani.../