Uhispania: Tutaendelea kuisaidia UN kifedha kuchunguza jinai za kivita zilizofanywa na Israel Ghaza
Uhispania itachangia yuro 500,000 (zaidi ya $560,000) kusaidia uchunguzi wa Umoja wa Mataifa kuhusu ukiukaji wa haki za binadamu na uhalifu wa kivita unaowezekana kuwa umefanywa huko Ghaza. Hayo yameelezwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uhispania Jose Manuel Albares.
Wiki iliyopita, Ismail Thawabteh, mkurugenzi wa ofisi ya vyombo vya habari vya serikali ya Ghaza, alivieleza vyombo vya habari kuwa, eneo hilo limeingia katika "hatua ya juu ya baa la njaa" kutokana na kuendelea kufungwa vivuko vya mpakani na mashambulizi mapya ya kijeshi yanayofanywa na utawala wa Kizayuni.
Zaidi ya Wapalestina 52,500 wengi wao wakiwa wanawake na watoto wameshauawa shahidi hadi sasa katika Ukanda wa Ghaza tangu jeshi la utawala ghasibu wa Israel lilipoanzisha vita vya kinyama na mauaji ya kimbari dhidi ya eneo hilo mnamo Oktoba 7, 2023.../