Naibu Katibu Mkuu wa UN ahimiza umoja na mshikamano wa walimwengu
https://parstoday.ir/sw/news/world-i22462-naibu_katibu_mkuu_wa_un_ahimiza_umoja_na_mshikamano_wa_walimwengu
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amewataka viongozi wa nchi zote duniani kuimarisha umoja na mshikamano na kujiepusha na hitilafu na mifarakano.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Dec 31, 2016 00:19 UTC
  • Naibu Katibu Mkuu wa UN ahimiza umoja na mshikamano wa walimwengu

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amewataka viongozi wa nchi zote duniani kuimarisha umoja na mshikamano na kujiepusha na hitilafu na mifarakano.

Jan Eliasson mbaye muda wake wa kuhudumu katika cheo hicho unamalizika kesho sambamba na kumalizika mwaka huu wa 2016 amesema umoja na mshikamano ndiyo haja kubwa zaidi ya dunia ya sasa na kuongeza kuwa, kuna haja ya kutafakari na kutafuta njia ya kutatua migogoro ya dunia kama suala la wahamiaji, wakimbizi na kusitishwa vita katika maeneo mbalimbali.

Jan Eliasson

Eliasson pia amewataka viongozi wa nchi mbalimbali kuacha tabia ya kusisitiza juu ya migawanyiko ya kiutaifa, kikabila au kidini. Adha amesisitiza umuhimu wa kuheshimiwa haki za binadamu.

Kuhusu suala lililomkatisha tamaa zaidi kama Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Jan Eliasson  amesema ni maafa ya Syria na kwamba Umoja wa Mataifa umeshindwa kukomesha mgogoro huo.

Wasyria wakigangaika kutafuta makimbilio

Amesema mgogoro wa Syria umesasababisha mauaji ya mamia ya maelfu ya binadamu na kuwalazimisha mamilioni ya wengine kuwa wakimbizi katika nchi nyingine. Amesisitiza kuwa mgogoro wa Syria umesababisha ukosefu wa uthabiti katika siasa za kimataifa.