Oct 30, 2019 10:19
Jumatano ya wiki hii tarehe Mosi Mfunguo Sita Rabiul Awwal ilisadifiana na siku ya Hijra ya Mtume wetu Muhammad (saw) kutoka Makka na kuhamia Madina na inakumbusha tukio maarufu la "Lailatul Mabiit', usiku ambao ndani yake Amirul Muuminin Ali bin Abi Twalib (as) alisabilia nafsi yake kwa kulala katika kitanda cha Mtume wakati mtukufu huyo alipoondoka Makka akielekea Madina.