-
Hizbullah ya Lebanon: Marekani ni adui mkuu wa Waarabu na Waislamu
Dec 18, 2017 14:34Mkuu wa Baraza la Kisiasa la Harakati ya Mapambano ya Hizbullah ya Lebanon amesisitiza kuwa, hii leo ulimwengu umefahamu na kudiriki kwamba, dola la Marekani ndio adui mkuu wa Waarabu na Waislamu.
-
Larijani: Israel inafanya njama za kuzusha vurugu za kisiasa katika Mashariki ya Kati
Dec 18, 2017 14:14Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, utawala dhalimu wa Israel unafanya njama za kuleta vurugu za kisiasa katika Mashariki ya Kati na kuongeza kuwa, endapo nchi za Kiislamu zitadumisha umoja na mshikamano zitazuia kufikiwa malengo hayo ya Wazayuni.
-
Utawala wa Kizayuni na utumiaji wa gesi za sumu dhidi ya Wapalestina
Dec 18, 2017 11:30Kitendo cha kiuadui cha rais wa Marekani, Donald Trump cha kuitangaza Quds tukufu kuwa eti ni mji mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel kimekiuka sheria na makubaliano yote ya kimataifa na kuandaa uwanja wa kufutwa kikamilifu taifa la Palestina katika uso wa dunia.
-
Saudia yapanga uhaini mwingine, mara hii ni kuiuzia Israel maeneo ya Palestina, Quds Tukufu ikiwemo
Dec 18, 2017 04:43Tovuti ya Intaneti ya Arabi 21 imefichua kuwa, mrithi wa ufalme wa Saudia anapanga njama kubwa ambayo mara hii inajumuisha kuiuzia Israel eneo la Palestina la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na mji wa Quds Tukufu (Jerusalem) uliko Msikiti wa Al Aqsa kwa mabilioni ya dola.
-
Kikao cha dharura cha kamati ya Palestina ya Muungano wa Mabunge ya Kiislamu kufanyika kesho Tehran
Dec 17, 2017 14:13Kikao cha dharura cha kamati ya Palestina ya Muungano wa Kimataifa wa Mabunge ya nchi za Kiislamu kinatarajiwa kufanyika kesho hapa mjini Tehran kwa kuhudhuriwa na Maspika wa Mabunge ya nchi tatu za Iran, Mali na Iraq.
-
Huenda Baraza la Usalama la UN likakutana kesho kujadili uamuzi wa Trump dhidi ya Quds
Dec 16, 2017 08:11Mwakilishi wa Palestina katika Umoja wa Mataifa amesema, kuna uwezekano kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la umoja huo kikafanyika hapo kesho kujadili rasimu ya azimio linalohusu uamuzi uliochukuwa na Marekani dhidi ya mji wa Baitul Muqaddas.
-
Sisitizo la kudumishwa mapambano ya Intifadha huko Palestina
Dec 15, 2017 17:18Maelfu ya wananchi wa Palestina jana Alkhamisi walikusanyika katika Medani ya al Katiba katika eneo la Ukanda wa Gaza wakipiga nara na kaulimbiu ya "Mapambano ni Uamuzi Wetu, na Umoja ni Chaguo Letu" na kuadhimisha mwaka wa 30 tangu kuasisiwa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS).
-
Wapalestina waandamana katika "Ijumaa ya Ghadhabu" dhidi ya Trump
Dec 15, 2017 17:02Raia wa Palestina leo Ijumaa wamefanya maandamano katika ardhi zote zinazokaliwa kwa mabavu chini ya anwani "Ijumaa ya Hasira" ili kulalamikia na kupinga hatua ya hivi karibuni ya Rais Donald Trump wa Marekani ya kuutangaza mji mtakatifu wa Quds kuwa mji mkuu wa Israel.
-
Tunisia yabadilisha jina la vituo vya TAXI na kuita Quds
Dec 15, 2017 04:18Chama cha wamiliki wa TAXI nchini Tunisia kimebadilisha jina la vituo vyake na kuviita Quds kama njia ya kulalamikia uamuzi wa Marekani wa kuitambua rasmi Quds kuwa eti ni mji mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Hamas: Hakuna nchi inayoitwa 'Israel' hata mji mkuu wake uwe 'Quds'
Dec 14, 2017 16:01Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas imelaani vikali uamuzi wa Rais wa Marekani, Donald Trump wa kuitangaza Baytul Muqaddas kuwa mji mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel na kusisitiza kuwa, hakuna dola linaloitwa Israel hata mji mkuu wake uwe Quds tukufu.