-
Mwakilishi wa Mayahudi katika bunge la Iran: Hatua ya Trump ya kuitambua Quds mji mkuu wa Israel ni ubaguzi wa kimbari
Dec 14, 2017 15:59Mwakilishi wa jamii ya wachache ya Mayahudi katika Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran amesema hatua ya rais wa Marekani ya kuitangaza Baitul Muqaddas mji mkuu wa utawala wa Kizayuni ni ubaguzi wa kimbari.
-
Erdogan: Israel ni dola vamizi na la kigaidi
Dec 13, 2017 16:13Rais Recep Tayyip Erdoğan wa Uturuki amesema kuwa, kuwa na nguvu na kumiliki silaha si dalili kuwa Marekani ina nguvu, na maamuzi yake yatasababisha matatizo makubwa katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Jumuiya ya NAM yakosoa hatua ya Marekani dhidi ya Quds
Dec 13, 2017 15:25Jumuiya ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote (NAM) imekosoa vikali hatua ya Rais Donald Trump wa Marekani ya kuitambua Quds kuwa eti mji mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Bunge la Iran: Quds ni kibla cha kwanza cha Waislamu na ni ya Umma wote wa Kiislamu
Dec 12, 2017 16:26Wabunge wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu, Bunge la Iran, wamesema uamuzi wa Rais wa Marekani kutambua Quds Tukufu (Jerusalem) kama mji mkuu wa utawala bandia wa Israel ni dalili ya wazi kabisa ya kutokuwa na utambulisho utawala huo wa Kizayuni.
-
Jenerali Qassem Soleimani: Iran iko tayari kuvisaidia vikosi vya Muqawama vya Palestina kwa kila hali
Dec 12, 2017 16:18Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) ametangaza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iko tayari kutoa msukumo na kuvisaidia kwa kila hali vikosi vya Muqawama wa Kiislamu wa Palestina.
-
Rais Rouhani kushiriki mkutano wa dharura wa OIC, Quds ndiyo ajenda kuu
Dec 12, 2017 08:19Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran leo anaelekea Uturuki kwa shabaha ya kushiriki katika kikao cha dharura cha viongozi wa nchi wanachama katika Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) nchini Uturuki.
-
Trump, White House watengwa kutokana na uamuzi dhidi ya Quds
Dec 12, 2017 08:17Katibu Mkuu wa Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Lebanon amesema kitendo cha Donald Trump cha kuitangaza Quds ambayo ina Kibla cha Kwanza cha Waislamu kuwa eti ni mji mkuu wa Israel imeifanya Ikulu ya White House na rais huyo wa Marekani watengwe kimataifa.
-
Rouhani: Mataifa ya Kiislamu yatazima njama ya Marekani na Israel
Dec 12, 2017 03:00Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema umoja, muqawama na mapambano ya Wapalestina na nchi nyingine za Kiislamu bila shaka yatapelekea kusambaratika kwa njama ya Marekani na utawala wa Kizayuni ya kuitambua Quds tukufu kuwa 'mji mkuu' wa utawala haramu wa Israel.
-
Larijani: Hatua ya Trump dhidi ya Quds ni kujaribu kuficha kushindwa Marekani katika eneo hili
Dec 12, 2017 02:37Mkuu wa Chombo cha Mahakama cha Iran amesema kuwa, kitendo cha rais wa Marekani, Donald Trump cha kuitangaza Quds ambayo ina Kibla cha Kwanza cha Waislamu kuwa eti ni mji mkuu wa Israel, ni kujaribu kuficha kufeli siasa za Marekani katika eneo hili.
-
Iran: Dunia imeungana kumlaani Donald Trump
Dec 11, 2017 14:49Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran leo amezungumza na waandishi wa habari kuhusiana na masuala mengi tofauti ikiwemo ziara ya waziri wa mambo ya nje wa Uingereza hapa mjini Tehran, suala la Quds, Yemen na masuala mengine mbalimbali.