-
Iran na Afrika Kusini kustawisha uhusiano wao wa kiulinzi
Oct 15, 2018 00:16Mkuu wa masuala ya kimataifa wa Wizara ya Ulinzi ya Iran na Waziri wa Ulinzi wa Afrika Kusini wamesisitizia kustawishwa ushirikiano wa kiulinzi na kijeshi kati ya nchi mbili.
-
Mjukuu wa Mandela: Utawala kandamizi wa Israel ni mbaya zaidi kuliko ule wa ubaguzi wa rangi
Oct 12, 2018 13:42Mjukuu wa shujaa wa uhuru wa Afrika Kusini Mzee Nelson Mandela amefananisha mauaji yanayofanywa na Israel dhidi ya waandamanaji wa Palestina huko katika Ukanda wa Gaza na mauaji yaliyofanywa na utawala wa ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini katika eneo la Sharpeville mwaka 1960 na kusisitiza kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel ni mbaya zaidi kuliko ule wa apartheid.
-
Iran na Afrika Kusini kuimarisha ushirikiano wa kiulinzi
Oct 12, 2018 01:03Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Afrika Kusini zimesisitiza juu ya azma zilionayo ya kuimarisha ushirikiano wa kiulinzi baina yao.
-
Afrika Kusini yatuhumiwa kushirikiana na Saudia katika mauaji ya watu wa Yemen
Oct 08, 2018 11:17Serikali ya Afrika Kusini imetuhumiwa kuwa inashirikiana na Saudi Arabia katika mauaji yanayofanywa na utawala huo wa kifalme dhidi ya raia wasio na hatia nchini Yemen.
-
Afrika Kusini yapongeza ushindi wa Iran dhidi ya Marekani katika mahakama ya ICJ
Oct 07, 2018 04:18Idara ya Uhusiano na Ushirikiano wa Kimataifa ya Afrika Kusini imepongeza hatua ya Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu (ICJ) kuiagiza Washington isimamishe vikwazo vyake vya upande mmoja dhidi ya Iran haraka iwezekanavyo.
-
Afrika Kusini yatakiwa kusitisha ushirikiano wake wa kijeshi na Saudia
Oct 04, 2018 23:33Wanaharakati wa masuala ya amani na haki za binadamu wa Afrika Kusini wameitaka serikali ya nchi hiyo isimamishe ushirikiano wake wa kijeshi na Saudi Arabia kutokana na ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu unaofanywa na utawala wa Riyadh hususan nchini Yemen.
-
Namibia kuwapokonya wazungu mashamba kama Afrika Kusini
Oct 04, 2018 10:41Rais wa Namibia ameahidi kwamba atatwaa mashamba ya kilimo yanayomilikiwa na Wazungu nchini humo na kuyagawa kwa wananchi wazalendo wa nchi hiyo.
-
Waafrika Kusini waandamana kupinga ukosefu wa amani
Oct 01, 2018 23:42Maandamano yaliyofanywa na wakazi wa jiji la Johannesburg nchini Afrika Kusini kulalamikia hali mbaya ya ukosefu wa usalama yamegeuka na kuwa ghasia na machafuko makubwa.
-
Afrika Kusini yakanusha taarifa za kurejea tena balozi wake mjini Tel Aviv
Sep 26, 2018 23:30Serikali ya Afrika Kusini imekanusha taarifa zilizoenea kwamba, imemrejesha huko Tel Aviv balozi wake ambaye ilimwita nyumbani mwezi Mei mwaka huu.
-
Rais wa Afrika Kusini atoa wito wa kupasishwa mkataba wa kuzuia silaha za nyuklia
Sep 26, 2018 00:36Rais wa Afrika Kusini amezitaka nchi zote duniani kutia saini mkataba wa kuzuia silaha za nyuklia wa mwaka 2017 TPNW kwa kifupi.