-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran yuko safarini Afrika Kusini
Oct 22, 2017 10:34Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Mohammad Javad Zarif leo amewasili Afrika Kusini katika safari yake ya kuzitimbelea nchi kadhaa za bara Afrika.
-
Mahakama ya Juu Afrika Kusini yaidhinisha kufunguliwa tena mashtaka 783 ya ufisadi dhidi ya Rais Zuma
Oct 14, 2017 11:58Mahakama ya Juu ya Rufaa nchini Afrika Kusini imeidhinisha kufunguliwa tena mashtaka yapatayo 800 ya ufisadi yaliyokuwa yakimkabili rais wa nchi hiyo Jacob Zuma kabla ya kuwa rais. Mashtaka hayo ya ufisadi yanahusu mkataba wenye thamani ya randi bilion 30, sawa na dola bilioni mbili wa mauzo ya silaha yaliyoihusisha serikali ambayo yalifanyika mwishoni mwa miaka ya 90.
-
Jumatano tarehe 11 Oktoba, 2017
Oct 10, 2017 22:59Leo ni Jumatano tarehe 20 Mfunguo Nne Muharram 1439 Hijria inayosadifiana na tarehe 11 Oktoba, 2017.
-
Iran na Afrika Kusini zaafikiana kuongeza ushirikiano wa mawasiliano na teknolojia ya habari
Sep 27, 2017 10:48Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Afrika Kusini zimekubaliana kuongeza kiwango cha ushirikiano wao katika uga wa mawasiliano na teknolojia ya habari.
-
Waafrika Kusini waandamana kulaani ufisadi chini ya Rais Zuma
Sep 27, 2017 10:43Maelfu ya wananchi wa Afrika Kusini wamefanya maandamano katika mji wa Cape Town kudhihirisha ghadhabu zao kutokana na kashfa mbalimbali za ufisadi, ukosefu wa ajira na kuzorota uchumi chini ya utawala wa Rais Jacob Zuma wa nchi hiyo.
-
Waziri wa Afrika Kusini akitaka chama ANC kimuadhibu Zuma
Sep 22, 2017 13:00Waziri wa Nyumba na Makazi wa Afrika Kusini, Lindiwe Sisulu leo amesema kuwa chama tawala nchini humo ANC kinapasa kumuadhibu Rais Jacob Zuma kwa kukisababishia chama hicho sifa mbaya.
-
Waafrika Kusini waandamana kupinga mauaji ya kimbari ya Waislamu, Myanmar
Sep 16, 2017 02:38Wananchi wa Afrika Kusini wamefanya maandamano wakilaani mauaji ya kimbari yanayofanyika nchini Myanmar dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya.
-
Iran na Afrika Kusini kuimarisha uhusiano wao wa Kibunge
Sep 12, 2017 10:30Hossein Amir-Abdollahian, Mkurugenzi Mkuu wa Masuala ya Kimataifa wa Bunge la Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu na Afrika Kusini zinaweza kutumia uwezo wao kuondoa vizuizi vilivyopo ili kuimarisha uhusiano wa pande mbili ukiwemo wa kibunge.
-
Juhudi za wapinzani wa serikali Afrika Kusini za kumuondoa madarakani Jacob Zuma
Sep 06, 2017 05:45Vyama vya upinzani nchini Afrika Kusini vimeanzisha mikakati mipya ya kumsaili na kumuondoa madarakani Rais wa nchi hiyo Jacob Zuma kwa kuwasilisha mashtaka katika Mahakama ya Katiba ya nchi hiyo.
-
Upinzani Afrika Kusini waanzisha jitihada mpya za kumuuzulu Zuma
Sep 05, 2017 23:11Vyama vya upinzani nchini Afrika Kusini vimeanzisha jitihada mpya za kumuondoa madarakani Rais Jacob Zuma wa nchi hiyo ambaye tayari anaandamwa na kesi chungu nzima za ufisadi na utumiaji mbaya wa mamlaka.