-
Answarullah: Kuna vita vikubwa vinakuja ndani ya ardhi ya Saudi Arabia
Jun 16, 2019 02:18Mjumbe mmoja mwandamizi wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Answarullah ya Yemen amesema kuwa, karibuni hivi kutaanza vita vikubwa ndani ya ardhi ya adui Saudi Arabia.
-
Answarullah: Operesheni za droni dhidi ya Saudia na Imarati zitaendelea
Jun 15, 2019 04:44Mohamed Albakhiti, Mjumbe wa Baraza la Kisiasa la Harakati ya Wananchi ya Answarullah nchini Yemen, amesema kuwa operesheni za kikosi cha anga na ndege zisizo na rubani (droni) zitaendelea hadi pale Saudia na Imarati zitakapohitimisha uvamizi wao.
-
Ansarullah ya Yemen: Jinai mpya Sana'a ni ishara ya kutokuwa na uwezo muungano vamizi wa Saudi Arabia
May 18, 2019 03:24Msemaji wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen amelaani jinai mpya za muungano vamizi wa Saudi Arabia na Imarati huko Sana'a na kusema kuwa, jinai hizo ni ishara ya wazi ya kutokuwa na uwezo muungano huo vamizi.
-
Answarullah: Baadhi ya tawala za Kiarabu zinaharakia kufutwa kadhia ya Palestina
Apr 22, 2019 13:33Msemaji wa Harakati ya Wananchi ya Answarullah nchini Yemen amesema kuwa, baadhi ya tawala za Kiarabu zina pupa ya kutaka kufutwa haraka kadhia ya Palestina, kuliko hata utawala adui wa Kizayuni.
-
Ansarullah yaafiki mpango wa kupeleka askari al Hudaydah
Feb 19, 2019 03:54Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Siasa la Yemen Mahdi al-Mashat amekutana na mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya nchi hiyo na kutangaza kuwa harakati ya Ansarullah imeafiki mpango wa kutumwa tena askari katika mji wa bandarini wa al Hudaydah.
-
Wayemen waandamana kulaani 'Waarabu Wasaliti'
Feb 17, 2019 13:56Makumi ya maelefu ya watu wa Yemen wameanadamana kote katika nchi hiyo kulaani nchi za Kiarabu ambazo zinatekeleza usaliti kwa kuanzisha mchakato wa kuwa na uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel.
-
Waziri wa Ulinzi wa Yemen: Karibuni hivi tutaingia hatua mpya ya mashambulizi dhidi ya Saudia
Jan 23, 2019 02:48Waziri wa Ulinzi wa Yemen, amesema kwamba jeshi na kamati za wananchi nchini humo wameweza kuboresha zana zao za kiulinzi na kwamba katika siku chache zijazo wataingia katika hatua mpya ya mashambulizi.
-
Harakati ya Ansarullah ya Yemen yasisitiza kuheshimu makubaliano ya Stockholm Sweden
Jan 11, 2019 08:07Mkuu wa Kamati Kuu ya Mapinduzi ya Yemen ameashiria kuheshimu na kufungamana Harakati ya Ansarullah na makubaliano ya ya Stockholm Sweden na kusema kuwa, muungano vamizi unaoongozwa na Saudi Arabia unapaswa kuheshimu na kutekeleza makubaliano hayo.
-
Ansarullah: Hakuna hatua iliyochukuliwa kwa ajili ya kusitisha mapigano al Hudaydah
Jan 09, 2019 07:03Afisa Uhusiano wa Nje wa harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema kuwa, hakuna hatua yoyote ya kivitendo iliyochukuliwa kwa ajili ya kutekeleza mapatano ya kusitisha mapigano katika mji wa bandari wa al Hudaydah magharibi mwa Yemen na kubadlishana mateka kwa mujibu wa makubaliano yaliyofikiwa mjini Stockholm, Sweden.
-
Ansarullah ya Yemen: Tunaheshimu mazungumzo ya Stockholm
Jan 07, 2019 04:24Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Uokovu wa Kitaifa ya Yemen amesema kuwa harakati ya Ansarullah ya nchini humo inaheshimu na kutekeleza makubaliano ya kusitisha uhasama na mapigano yaliyofikiwa huko Stockholm nchini Sweden.