-
SAUTI, EAC: Tutatuma waangalizi wa uchaguzi nchini Burundi, pia yaipongeza serikali ya Bujumbura kwa maandalizi mazuri
Feb 11, 2020 04:07Jumuia ya Afrika imepanga kuwatuma waangalizi wake kwa ajili ya kufuatilia zoezi la uchaguzi ujao nchini Burundi.
-
SAUTI, Majina ya wagombea wanaotaka kumrithi Rais Nkurunziza nchini Burundi, yawekwa wazi
Feb 03, 2020 12:53Wagombea 10 wa kiti cha urais katika uchaguzi wa rais uliopangwa kufanyika tarehe 20 Mei mwaka huu, tayari wamefamika.
-
Chama tawala nchini Burundi chamteua mgombea wa urais
Jan 26, 2020 09:31Chama tawala cha CNDD-FDD nchini Burundi kimemteua Katibu Mkuu wa chama hicho, Evariste Ndayishimiye kuwa mgombea wa kiti cha urais wa chama hicho katika uchaguzi mkuu unaotazamiwa kufanyika mwezi Mei mwaka huu.
-
Wakazi wa kaskazini mwa Bujumbura waendelea kuteseka kwa madhara ya mafuriko + Sauti
Jan 07, 2020 05:01Waathiriwa wa mafuriko katika baadhi ya maeneo ya kaskazini mwa Bujumbura waliopiga kambi katika madarasa ya shule wametakiwa kuondoka ili kuruhusu sehemu ya pili ya mwaka wa shule kuanza. Hata hivyo raia hao wanalalamika kutokuwa na sehemu ya kwenda. Hali hiyo imepelekea baadhi ya shule katika eneo hilo kuakhirisha kufungua muhula mpya wa masomo. Hamida Issa na maelezo zaidi kutoka Bujumbura…
-
SAUTI, Shirika la Kutetea haki za Wafungwa nchini Burundi NDABARIZA lataka msamaha wa Rais Nkurunziza utekelezwa haraka
Jan 02, 2020 13:32Shirika la Kutetea Haki za Wafungwa nchini Burundi (NDABARIZA), limevitaka vyombo husika vya serikali kutekeleza agizo la Rais Pierre Nkurunziza la kuwaachilia huru wafungwa waliopewa msamaha na rais huyo.
-
Idadi ya waliokufa kutokana na mafuriko Burundi yafika 43, Uganda 22
Dec 08, 2019 08:40Idadi ya watu walipoteza maisha kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika nchi kadhaa za Afrika Mashariki imeongezeka.
-
SAUTI, Wafanyabiashara wa jiji la Bujumbura waitaka serikali iwaonee huruma kutokana na amri ya meya wa mji huo
Nov 28, 2019 13:13Baada ya Meya wa jiji la Bujumbura Freddy Mbonimpa, kutangaza operesheni ya hatua 10 alizozitaja kama njia yenye lengo la kuinuwa uchumi na kuimarisha usalama mjini hapo, tayari polisia imeanzisha msako wa kuwakamata machinga wanaojishughulisha katika maeneo ambayo hayajaratibiwa kufanyia shughuli hizo.
-
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Burundi atembelea eneo aliloshambuliwa na waasi + Sauti
Nov 25, 2019 12:34Wiki moja baada ya kushambuliwa na watu wenye silaha walotajwa na jeshi la Burundi kwamba walitokea katika nchi jirani ya Rwanda, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Burundi, Pascal Barandagiye, ametembelea tarafa ya Mabayi na kuwataka raia na watawala kuwa makini juu ya suala la usalama wakati huu ambapo imebakia miezi 6 tu kabla ya kufanyika uchaguzi nchini Burundi. Hamida Issa na maelezo zaidi kutoka Bujumbura.
-
Burundi: Waasi wa Rwanda ndio wamewaua askari wetu 8 na kuwajeruhi wengine
Nov 19, 2019 12:56Wizara ya Ulinzi pamoja na duru za kijeshi za Burundi zimetangaza kwamba askari wanane wa nchi hiyo wameuawa katika shambulio lililotokea karibu na mpaka wa Rwanda.
-
Watu 3 wauawa katika shambulio la mtutu wa bunduki Bujumbura, Burundi
Nov 02, 2019 09:24Watu waliojizatiti kwa silaha huku wakiwa wamevalia magwanda ya jeshi na polisi wameshambulia klabu moja ya burudani na kuua watu watatu katika mji mkuu wa zamani wa Burundi, Bujumbura.