-
Sierra Leone yapongeza msaada endelevu wa China kwa maendeleo ya miundombinu ya nchi hiyo
Mar 10, 2024 08:23Rais Julius Maada Bio wa Sierra Leone amepongeza msaada endelevu wa China kwa nchi yake katika maendeleo ya miundombinu ya nchi hiyo. Rais Bio ameeleza haya katika mahojiano aliyofanyiwa alipokuwa katika ziara ya kiserikali nchini China.
-
China yaunga mkono Palestina kuwa mwanachama kamili wa Umoja wa Mataifa
Mar 07, 2024 08:34Waziri wa Mambo ya Nje wa China amesema nchi yake inaunga mkono Palestina kupewa uanachama "kamili" wa Umoja wa Mataifa na kuongeza kuwa takwa la muda mrefu la watu wa Palestina la kuanzisha nchi yao huru haliwezi kuepukika tena.
-
Russia, China: US inahatarisha usalama wa Asia Magharibi
Feb 06, 2024 07:30Russia na China zimelaani vikali mashambulizi ya anga ya Marekani dhidi ya Iraq na Syria na kusisitiza kuwa, Washington ni tishio kwa usalama wa eneo zima la Asia Magharibi.
-
Ansarullah: US kuiasa China iingilie kadhia ya Bahari Nyekundu ni ishara ya kufeli
Feb 02, 2024 04:19Kiongozi wa Harakati ya Muqawama ya Ansarullah ya Yemen amesema juhudi za Washington za kutafuta usaidizi na upatanishi wa China ili iwaombe Wayemen wasimamishe mashambulizi dhidi ya meli za Marekani na Uingereza zinazopita Bahari Nyekundu zinaonesha namna madola hayo mawili ya kibeberu yalivyofeli katika mipango yao.
-
Upinzani wa China kwa hatua ya Marekani ya kuishambulia kijeshi Yemen
Jan 26, 2024 23:04Wang Wenbing, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China amesema, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa halijatoa kibali kwa mtu yeyote kutumia nguvu dhidi ya Yemen, akimaanisha hujuma na mashambulio ya kijeshi yanayofanywa na Marekani na Uingereza dhidi ya ngome na vituo vya harakati ya Ansarullah ya Yemen.
-
China yatoa tahadhari ya kuibuka tena mripuko wa COVID-19 kupitia spishi ya aina nyingine
Jan 16, 2024 03:24Maafisa wa Afya nchini China wametahadharisha juu ya uwezekano wa kuibuka tena mripuko wa ugonjwa wa COVID-19 katika mwezi huu wa Januari, utakaochochewa na kuongezeka maambukizi ya spishi mpya ya JN.1.
-
Ombi la serikali ya China kwa watu wa Taiwan
Jan 12, 2024 23:17Serikali ya China imewataka watu wa kisiwa cha Taiwan kutompigia kura William Lai, mgombea mkuu wa uchaguzi wa urais katika kisiwa hicho.
-
China yaijuza Marekani kwamba 'haitalegeza msimamo katu' juu ya Taiwan
Jan 10, 2024 02:49China imeapa kutekeleza bila kuyumbayumba msimamo wake wa kuiunganisha tena Taiwan na ardhi kuu ya nchi hiyo na kuitaka Marekani iache kukipatia silaha kisiwa hicho na kupunguza harakati zake katika Bahari ya China Kusini.
-
China yayawekea vikwazo makampuni matano ya Marekani kwa kuiuzia silaha Taiwan
Jan 08, 2024 03:09Wizara ya Mambo ya Nje ya China imetangaza vikwazo dhidi ya makampuni matano ya Marekani kwa kuiuzia Taiwan silaha.
-
Beijing yaionya Taipei huku uchaguzi ukikaribia kufanyika katika kisiwa cha Taiwan
Jan 05, 2024 04:14Huku uchaguzi mkuu wa rais na bunge ukikaribia kufanyika huko Taiwan tarehe 13 January, kiongozi wa ngazi ya juu ya China ameutaja uchaguzi huo kuwa chaguo kati ya vita na amani.