-
Kuachiliwa huru wapinzani wa serikali ya Ethiopia; juhudi za kuanzisha mazungumzo ya kitaifa
Jan 09, 2022 23:21Baada ya miezi kadhaa ya mzozo na vita nchini Ethiopia, Abiy Ahmed Waziri Mkuu wa nchi hiyo ametangaza msamaha na kuwaachia huru wafungwa mashuhuri wa kisiasa akiwemo kiongozi wa upinzani Jawar Mohammed na maafisa wa chama cha upinzani cha Tigray na hivyo kupiga hatua ya kwanza kwa minajili ya kurejesha utilivu wa kisiasa na kuandaa uwanja kwa ajili ya mazungumzo ya kitaifa.
-
Shambulizi ya anga laua wafanyakazi 56 wa misaada ya kibinadamu Tigray
Jan 09, 2022 01:16Shambulio la anga katika eneo la Tigray nchini Ethiopia limesababisha vifo vya watu 56 na kujeruhi wengine 30 wakiwemo watoto, katika kambi ya watu waliokimbia makazi yao. Hayo yamesemwa na wafanyakazi wawili wa kutoa misaada wakinukuu mamlaka za eneo hilo na watu walioshuhidia maafa hayo.
-
Ethiopia yatangaza msamaha kwa wafungwa wa kisiasa akiwemo kiongozi wa upinzani
Jan 08, 2022 03:40Serikali ya Ethiopia imetangaza kuwa itatoa msamaha na kuwaachia huru wafungwa mashuhuri wa kisiasa akiwemo kiongozi wa upinzani Jawar Mohammed na maafisa wa chama cha upinzani cha Tigray.
-
Katibu Mkuu wa UN akaribisha hatua chanya zilizochukuliwa na pande zinazopigana nchini Ethiopia
Dec 25, 2021 09:39Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amekaribisha tangazo la serikali ya Ethiopia kwamba jeshi lake litasitisha mashambulizi katika eneo ambako liko hivi sasa.
-
Ethiopia: Hatuna nia ya kuwashambulia waasi wa Tigray
Dec 22, 2021 09:39Serikali ya Ethiopia imetangaza kuwa, haina nia ya kuendeleza mashambulizi dhidi ya waasi wa Harakati ya Ukombozi wa Watu wa Tigray (TPLF).
-
Waasi wa Tigray warudi nyuma na kuondoka maeneo waliyokuwa wakiyadhibiti
Dec 20, 2021 23:05Mkuu wa Harakati ya Ukombozi ya Watu wa Tigray (TPLF) ametangaza kuwa, wapiganaji wa harakati hiyo wamerudi nyumana kuondoka katika maeneo yote nje ya eneo la Tigray huko kaskazini mwa Ethiopia ikiwa ni katika kujibu maombi ya kimataifa na kutoa fursa ya kurejesha amani katika eneo hilo.
-
Ethiopia: Baraza la Haki za Binadamu la UN linatumika kisiasa
Dec 18, 2021 00:04Ethiopia imekosoa kufanyika kwa kikao maalumu cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kujadili na kutathmini visa vya ukiukaji wa haki za binadamu nchini humo kufuatia mzozo unaoendelea kati ya serikali na waasi wa Tigray.
-
Watu 28 wauawa katika mashambulizi ya jeshi la Ethiopia
Dec 17, 2021 04:03Vyombo vya habari vimewanukuu wanamgambo wa kundi la Harakati ya Ukombozi wa Watu wa Tigray wakisema kuwa mashambulizi ya anga ya ndege za jeshi la Ethiopia yameua watu 28 na kujeruhi wengine 76 katika mji mmoja wa kaskazini mwa nchi hiyo.
-
Mgogoro wa Ethiopia kujadiliwa kwenye kikao cha dharura cha Baraza la Haki za Binadamu la UN
Dec 15, 2021 23:57Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa litakutana mjini Geneva kesho Ijumaa kwa kikao cha dharura kitakachojadili uhalifu wa kivita unaofanywa na pande zinazopigana nchini Ethiopia.
-
Abiy Ahmed arejea Addis Ababa kutoka kwenye medani ya vita, Ethiopia yajiandaa kushambulia ngome za mwisho za waasi wa Tigray
Dec 08, 2021 10:57Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed, ametangaza leo Jumatano kwamba amerejea Addis Ababa kutoka kwenye medani ya vita, na kuahidi kuendeleza vita dhidi ya kundi la Tigray People's Liberation Front (TPLF).