-
Radiamali ya China kuhusu kura ya turufu ya Marekani dhidi ya azimio la kusitisha vita Gaza
Dec 10, 2023 02:24Zhang Jun, mwakilishi wa kudumu wa China katika Umoja wa Mataifa, ameitaja kura ya turufu ya Marekani dhidi ya azimio la kusitisha mapigano huko Gaza kuwa imeweka wazi siasa za kundumakuwili za Washington katika uwanja wa kimataifa.
-
Safari ya Rais Vladimir Putin wa Russia katika nchi za Imarati na Saudi Arabia
Dec 09, 2023 02:42Rais Vladimir Putin wa Russia Jumatano alifanya ziara ya siku moja katika nchi za Imarati na Saudi Arabia ambapo alijadiliana na viongozi wa nchi hizo kuhusiana na uhusiano wa pande mbili na masuala ya kimataifa, vikiwemo vita vya Gaza.
-
Barua isiyo ya kawaida ya Guterres kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya Gaza
Dec 07, 2023 08:28Katika hatua isiyo ya kawaida, Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametumia mamlaka aliyopewa kisheria kupitia kifungu cha 99 cha Hati ya Umoja wa Mataifa kulishinikiza Baraza la Usalama la umoja huo lianzishe haraka usitishaji vita huko katika Ukanda wa Gaza.
-
Guterres atumia Ibara nadra ya UN kutuma ujumbe mzito kwa Baraza la Usalama kuhusu Gaza
Dec 07, 2023 03:36Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametumia ibara ya 99 ya Hati ya Umoja wa Mataifa, ambayo ni nadra sana kutumiwa na Katibu Mkuu wa umoja huo, kulitolea wito mzito Baraza la Usalama wa "kushinikiza kuepusha janga la kibinadamu" katika Ukanda wa Gaza na kuungana katika kutoa wito wa kusitishwa kikamilifu mapigano kati ya utawala wa Kizayuni wa Israel na Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS.
-
Wawakilishi wa Hamas washiriki katika kumbukumbu ya kumuenzi Mandela
Dec 06, 2023 05:53Maafisa wakuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) jana Jumanne waliungana na familia ya Nelson Mandela katika kumbukumbu ya miaka 10 ya kifo cha rais huyo wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, mjini Pretoria.
-
Waislamu Marekani waapa "kumdampu" Biden katika uchaguzi wa 2024 kwa sababu ya uungaji mkono wake kwa mauaji ya Israel
Dec 03, 2023 23:29Waislamu katika majimbo muhimu ya Marekani wamezindua kampeni ya #AbandonBiden kutokana na kukataa kwa rais huyo wa Merekani kutoa wito wa kusitishwa mashambulizi ya kinyama ya Israel huko Ukanda wa Gaza.
-
Amir-Abdollahian: Uwepo wa dola la Kizayuni umeitia kwenye matatizo makubwa dunia
Dec 02, 2023 07:15Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, jinai zinazoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni kwenye Ukanda wa Ghaza zimeiweka kwenye alama ya kuuliza itibari ya jamii ya kimataifa na madai ya kupigania haki za binadamu ulimwenguni.
-
Yemen: Silaha zetu zitaendelea kuupiga utawala wa Kizayuni wa Israel
Dec 02, 2023 07:12Mjumbe wa ngazi za juu wa Baraza Kuu la Kisiasa la Yemen amesema kuwa, silaha za nchi yake zimeelekezwa kwa adui Mzayuni ambaye ndiye adui nambari moja na kwamba utaendelea kuzitumia silaha hizo kuupiga utawala huo dhalimu.
-
Mauaji ya Wapalestina wa Gaza "yamvutia" Gallant alipoona wanavyoshambuliwa kutokea angani
Dec 02, 2023 02:35Waziri wa vita wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel Yoav Gallant amesema, jana alisafiri kwa helikopta ya kivita katika Ukanda wa Gaza kuangalia mashambulizi ya jeshi la utawala huo, ambayo yalianza tena asubuhi baada ya Tel Aviv kutangaza kumalizika usitishaji mapigano wa wiki moja kwa sababu za kibinadamu.
-
Erdogan: Netanyahu ni chinjachinja wa Gaza anayetaka kurefusha maisha yake ya kisiasa
Nov 30, 2023 22:58Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, amemtaja Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, kuwa ni "mchinjaji wa Gaza," akisisitiza kwamba anarikodi jina lake katika historia kwa sifa hiyo kwa sababu "amefanya moja ya ukatili mkubwa zaidi wa karne hii."