-
Pretoria: Tunatiwa wasi wasi na mauaji ya kigaidi ya Israel
Sep 29, 2024 10:45Afrika Kusini imetoa wito wa kusitishwa kwa mapigano mara moja nchini Lebanon, ambapo utawala wa Kizayuni wa Israel ulianza mashambulio ya anga hivi karibuni, na kuua mamia ya raia huku maelfu ya wengine wakilazimika kuyahama makazi yao.
-
Kiongozi Muadhamu: Wanamuqawama wa Palestina na Hizbullah ya Lebanon ndio washindi
Sep 25, 2024 10:30Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameonana na wanaharakati wa Vita vya Kujihami Kutakatifu na Muqawama na kusisitiza kuwa, kambi ya Muqawama ya Palestina na Hizbullah ya Lebanon ndiye mshindi.
-
Nasrullah: Adui Mzayuni amevuka mistari yote myekundu
Sep 19, 2024 23:02Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Hizbullah ya Lebanon Sayyid Hassan Nasrullah amesema maadui wa Kizayuni walivuka mistari yote myekundu siku ya Jumanne kwa kufanya jinai ya kuogofya katika nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Shambulio la kigaidi la Israel kusini mwa Lebanon laua shahidi mtu mmoja na kujeruhi wengine 13
Sep 14, 2024 07:01Mtu mmoja ameuawa shahidi na wengine 13 kujeruhiwa katika mashambulio la kigaidi la utawala wa kigaidi wa Israel huko kusini mwa Lebanon.
-
Hizbullah: Adui hana chaguo jingine ghairi ya kusitisha vita Gaza
Sep 08, 2024 09:26Mjumbe wa Baraza Kuu la Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, adui ana njia moja pekee, ambayo ni kusimamisha hujuma na mashambulizi ya kinyama dhidi ya Ukanda wa Gaza.
-
Idadi ya vifo Ghaza yapindukia 40,900 baada ya jeshi la Israel kuua Wapalestina wengine 61
Sep 07, 2024 08:22Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limewaua shahidi Wapalestina wengine 61 katika mashambulizi kwenye Ukanda wa Ghaza, na kuongeza idadi ya vifo kufikia 40,939 tangu Oktoba 7, 2023. Hayo ni kulingana na taarifa iliyotolewa leo na Wizara ya Afya ya Ghaza.
-
Walowezi wa Kizayuni wapiga muziki na kufanya ibada zao kwenye eneo la Msikiti wa Ibrahimi
Sep 03, 2024 23:09Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limeruhusu maelfu ya walowezi haramu kufanya tamasha la muziki na ibada zao katika eneo la Msikiti wa Ibrahimi ulioko kwenye mji wa Al-Khalil, Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan unaokaliwa kwa mabavu baada ya kuufunga Msikiti huo usitumiwe na Waislamu Wapalestina.
-
Palestina kuwasilisha ombi la kujiunga na BRICS baada ya mkutano wa Oktoba
Aug 27, 2024 03:28Palestina itawasilisha ombi la kujiunga na jumuiya ya kiuchumi ya BRICS baada ya mkutano wa kilele wa jumuiya hiyo unaotarajiwa kufanyika nchini Russia mwezi Oktoba. Hayo yameelezwa na balozi wa Palestina mjini Moscow Abdel Hafiz Nofal.
-
Mwangwi wa kikanda na kimataifa wa Operesheni ya Siku ya Arubaini na shambulizi la Hizbullah ya Lebanon dhidi ya utawala wa Kizayuni
Aug 26, 2024 22:40Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imedhihirisha uwezo wake katika nyanja mbalimbali na taathira yake kieneo na kimataifa dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel kwa operesheni ya Siku ya Arubaini ya Imam Hussein (as).
-
Hizbullah yakitwanga makombora kituo cha anga cha Israel, yateketeza mitambo ya ujasusi
Aug 23, 2024 23:05Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon imekishambulia kwa makombora kadhaa kituo cha uongozaji wa shughuli za anga cha Meron cha utawala wa Kizayuni wa Israel na kubomoa mitambo ya ujasusi ya kituo hicho.